August 31, 2016
Septemba mosi mwaka huu inataraji kuingia katika historia ya Tanzania
Septemba mosi mwaka huu inataraji kuingia katika historia ya Tanzania kutokana na matukio ambayo yanataraji kufanyika siku hiyo, matukio hayo ni pamoja na sherehe za miaka 52 ya Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ), maandamano ambayo yamepangwa kufanywa ya UKUTA na tukio la kupatwa kwa jua.
Akizungumza na Waandishi wa Habari wakati alipokutana na Maafisa wa Jeshi la JWTZ Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alisema JWTZ inapotimiza miaka 52 ni fahari kubwa hivyo tunapaswa kuwapongeza kwa kudumisha amani na mshikamano.
Alisema Jeshi hilo limejipanga kurusha angani ndege zake za kivita katika anga la Dar es Salaam, Septemba 1 mwaka huu, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 52 ya kuanzishwa kwake.
Makonda aliwataka wananchi kutokuwa na hofu wanaposikia ngurumo za ndege hizo bali wafurahie kwani ni ndege zao.
“Mnaposikia milio ya ndege zetu mbalimbali, mfurahie kwa sababu hizo ni ndege za wananchi. Usisikie muungurumo ukashtuka. Hakuna jambo lolote lile zaidi ya kuonesha vifaa vyetu na jinsi ambavyo wanajeshi wetu kwa miaka 52 wamaeendelea kuwa imara na vifaa vizuri,” alisema Makonda.
Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa waliwataka wananchi waliojipanga katika vikundi mbalimbali kuripoti kwa wakuu wao wa wilaya kujiandikisha ili waweze kushiriki pamoja na Jeshi hilo katika zoezi la usafi jijini humo.
Aliwataka wakazi wa mkoa huo pia kujitokeza kuchangia damu katika vituo mbalimbali ambavyo vimeanishwa ili kuunga mkono juhudi za uchangiaji damu zitakazofanywa na wanajeshi wa JWTZ.
“Hii ni sehemu ya amani, tufanye usafi kwa amani. Tujitolee damu zetu kwa amani na mwisho wa siku tuwaenzi na kuwapongeza wanajeshi wetu kwa kazi kubwa wanayoifanya,” Makonda alieleza.
Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa aliendelea kutoa onyo kwa watu watakaotaka kufanya maandamano yaliyopigwa marufuku ya oparesheni UKUTA akiwataka kutii sheria.
“Mimi ninavyojua UKUTA ni kuwa mtu amefika mwisho wa kufikiri sasa kama watakuwa wamefika mwisho wa kufikiria basi sisi tutawasaidia … watu wapo wanapanga kufanya mambo ya kusaidia jamii wao wanapanga maandamano nawashauri wananchi waungane na Polisi,” alisema Makonda.
Mmoja wa makamanda wa IS auawa nchini Syria
KALI ZOTE BLOG
Kundi la wapiganaji la Islamic state limetangaza kuwa mmoja wa kamanda wake mwandamizi ambae ni msemaji wa kundi hilo, Abu Muhammad al-Adnani ameuwawa nchini Syria.
Taarifa ya mtandao unaohusiana na kundi hilo Amaq, inasema kuwa Abu Muhammad ameuwawa wakati alipokuwa kwenye operesheni za kijeshi katika jimbo la Allepo.
Mtandao huo haukutoa taarifa nyengine zaidi.
Wanajeshi wa marekani wamethibitisha kuwa walikuwa wamemlenga Abu Muhammad al-Adnani lakini wanasema bado walikuwa wakichunguza matokeo ya shambulizi la anga la siku ya Jumanne katika mji wa Al-Bab, kaskazini mashariki ya jimbo la Allepo.
Marekani inamuelezea Abu Muhammad al-Adnani kuwa ni mpangaji mkuu wa mashambulizi ya nje ya I-S na imesema kuwa kifo chake kinaweza kuwa nukta muhimu ya kushindwa kwa kundi hilo.
Diamond Platnumz anunua Rolls Royce ya $400,000 na zaidi?
Kwa muda mrefu, staa huyo amekuwa akisema kuwa hilo ndilo gari analotaka kulimiki kiasi cha kujipa jina ‘The Rolls Royce Musician From East Africa.’
Diamond ambaye yupo jijini Los Angeles, Marekani alikoenda kushoot video ya wimbo aliomshirikisha Ne-Yo, ameshare kipande cha video kwenye Instagram cha gari hilo na kuashiria kuwa huenda akawa amelinunua tayari.
Hata hivyo hajasema iwapo gari hilo limeshakuwa mali yake ama alikuwa tu showroom kuosha macho!
Rolls Royce, ni magari yanayozalishwa na kampuni ya Uingereza na yalianzishwa na Charles Stewart Rolls na Sir Frederick Henry Royce, March 1906. Bei yake huanzia $300,000 – $500,000.
“Nataka nibadilishe aina ya gari sababu imekuwa ni muda mrefu, nafikiri ni muda wa kuwa na gari nililokuwa nalitamani siku zote, gari la ndoto yangu ni Rolls royce na ndio ninalotaka kulinunua mwaka huu wa 2016 na litakuwa na jina la PLATNUMZ na sio namba za kawaida,” aliiambia tovuti ya Millard Ayo miezi kadhaa iliyopita.
Alidai kuwa kwa alipofikia ni muhimu kwa na gari la hadhi yake ili kujiongezea thamani zaidi.
“Ndio maana nikipata Rolls Royce inatengeneza heshima,” alisema.
Hemedy PHD apata mtoto kwenye siku yake ya kuzaliwa
Hemedy PHD atashare siku yake ya kuzaliwa na mwanae.

Muimbaji na muigizaji huyo wa filamu, Jumanne hii, October 30 amesherehekea siku yake ya kuzaliwa na pia kuzaliwa kwa mwanae.
Akishare picha hiyo juu, Hemedy aliandika kwenye Instagram: YOU GOD FOR THE BLESSINGS!! HAPPIEST&LUCKIEST MAN ALIVE!! HAPPY TO BE UR FATHER! HAPPY TO SHARE THE SAME BIRTHDAY WITH MY OWN BLOOD!DAMN WE MADE HISTORY.”
“WELCOME TO THE WORLD BABY, THE NEW VERSION OF ME! MY LEGACY! 30TH AUGUST#ProudDad #FatherOftheYear #VIRGOCHOSEN. HAPPY BIRTHDAY TO US,” aliongeza.
Chris Brown akamatwa kwa ‘kumtishia’ mwanamke
KALI ZOTE BLOG
Polisi nchini Marekani wamemkamata na kumzuilia mwanamuziki mashuhuri Chris Brown kwa tuhuma za kushambulia mtu kwa silaha hatari.
Polisi waliitwa makazi ya Chris Brown na mwanamke aliyeomba msaada saa tisa usiku wa kuamkia leo.
Malkia wa urembo, Baylee Curran ameambia gazeti la LA Times, kwamba mwanamuziki huyo alimwelekezea mtutu wa bunduki.
Hata hivyo walizuiwa kuingia na ilibidi wasubiri hadi kupata idhini ya jaji kabla kufanya msako wa kutafuta bunduki katika makaazi hayo.
Mwanamke huyo aliyewaita polisi baadaye aliambia vyombo vya habari kwamba walitofautiana na Brown kuhusu majohari.
Alisema alikuwa ameingia kwa Bw Brown akiwa na rafiki yake na mshirika wa kibiashara na alikuwa akiangalia mkufu wa thamani uliokuwa umevaliwa na mwanamume mmoja pale mwanamuziki huyo alipomkaripia na kumtaka aondoke mara moja akiwa amemwelekezea bunduki.
Alifanikiwa kuondoka makazi hayo bila madhara.
Chris Brown ameandika ujumbe kwenye mitandao ya kijamii kujitetea na kuwalaumu polisi kwa kumhangaisha.
Wakili wake alifika kwenye makaazi hayo na kumsihi aandamane na maafisa wa polisi. Mwanamziki huyo anatarajiwa kufunguliwa mashtaka ya uvamizi.
Chris Brown amewahi kujipata matatani awali, hususan alipomshambulia aliyekuwa mpenzi wake na mwanamziki Rihanna hapo Februari 2009.