June 18, 2018

Unaweza usiipende sura ya Magufuli”- RC Mongella





Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella, amesema kuwa hakuna sababu ya msingi kwa mtu yeyote nchini ambaye ana hoja za kutilia shaka utendajikazi wa Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli labda kuwe na sababu nyingine ambazo ni nje ya utendajikazi.

Mongella ameongea hayo Juni 17, 2018 wakati wa uzinduzi wa kivuko kipya cha MV Mwanza ambacho kitafanyakazi katika eneo la Kigongo-Busisi, na kuongeza kuwa Serikali ya awamu ya tano imefanikiwa kufanya mambo makubwa katika kipindi cha muda mfupi tangu kuingia madarakani chini ya Rais Magufuli.
“Unaweza kumsema Magufuli labda hupendi sura yake, lakini huna namna ya kusema huyu mtu hafanyikazi, Serikali inapiga kazi leo tunaona meli MV Mwanza itaenda pale Kigongo feri kwenda Busisi ina uwezo mkubwa, ni jambo kubwa hii meli ni ya kisasa zaidi ni nyepesi, ina kwenda kasi na inabeba mzigo mkubwa” amesema Mongella
Mongella ameongeza kuwa kivuko hicho cha kisasa kitasaidia ufanisi katika sekta ya usafiri wa majini katika ziwa victoria kwasababu itasafirisha mizigo mikubwa kwa wakati mmoja na kwa gharama nafuu na kuwataka wananchi kuunga mkono jitihada za maendeleo zinazofanywa na Rais Magufuli.
Kivuko cha MV Mwanza kina uwezo wa kubeba uzito wa tani 250, kitafanya kazi katika eneo la Kigongo–Busisi Mkoani Mwanza na utengenezaji wake umegharimu jumla ya shilingi bilioni 8 na kitaweza kubeba abiria 1000 na magari 36 kwa wakati mmoja



Mike Kalambay   Belela

Kombe la Dunia 2018: Makundi yalivyo na ratiba ya mechi

Image result for kombe la dunia

Michuano ya Kombe la Dunia ya Fifa ya mwaka 2018 inaendelea nchini Urusi.
Michuano hiyo itashirikisha mataifa 32, wakiwemo mabingwa watetezi Ujerumani, na itakuwa na mechi 64 zitakazochezwa katika kipindi cha siku 32.
Fainali itachezwa 15 Julai.
Fainali za sasa za Kombe la Dunia ambazo ni za 21 zitachezwa katika viwanja 12 katika miji 11 nchini Urusi, ambayo inapatikana eneo la upana wa maili zaidi 1,800.
Kutokana na hili, kutakuwa na tofauti kubwa katika wakati mechi zinachezwa.
Ujerumani, waliowashinda Argentina katika fainali ya Kombe la Dunia 2014, wanapania kuwa taifa la kwanza kushinda kombe hilo mtawalia kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1962.
Hapa ni mwongozo wa makundi yalivyo na mechi zitakavyochezwa hatua ya makundi:

Kundi A
Kundi B

Brazil wanatafuta kuweka rekodi nyingine kwa kushinda kombe hilo kwa mara ya sita.
Michuano hiyo ya mwezi mmoja inatarajiwa kuwavutia mashabiki nusu milioni kwenda Urusi na kote duniani inatarajiwa kutazamwa na watu zaidi ya bilioni tatu.

Kundi C
Kundi D

Kuna makundi manane, kila kundi likiwa na timu nne.
Timu mbili ambazo zitamaliza juu kwenye kundi ndizo zitakazosonga hadi hatua ya 16 bora.
Fainali itachezewa katika uwanja wa Luzhniki ambao hutoshea mashabiki 81,000 mnamo 15 Julai.

Kundi E
Kundi F

Nani atashinda Kombe la Dunia?

Mabingwa watetezi Ujerumani, mabingwa mara tano Brazil, washindi wa Euro 2016 Ureno, waliomaliza wa pili 2014 Argentina, Ubelgiji, Poland na washindi wa mwaka 1998 Ufaransa ni timu nane ambazo zilikuwa kwenye chungu wakati wa kufanywa kwa droo.
Wote wanapigiwa upatu kushinda.

Kundi G
Kundi H

Unaweza kusoma pia:





Mike Kalambay   Belela

Hakuna binadamu kama Ronaldo tokea dunia kuumbwa

.

Mkuu wa Habari na Mawasiliano wa Mabingwa wa Ligi Kuu (VPL) Simba SC, Haji Manara amefunguka na kumwagia sifa nyota wa timu ya Taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo huku akidai mchezaji huyo ndio mtu maarufu ulimwenguni kote na mtu pekee aliyepigwa picha nyingi tokea alipoumbwa Adam na Hawa

Manara ametoa kauli hiyo asubuhi ya leo Juni 16, 2018 baada ya Ronaldo kuingia kwenye 'record' ya kuwa mfungaji wa kwanza kufunga Hat- Trick ya kwanza katika fainali za Kombe la Dunia 2018 kwenye mechi ya Kundi B iliyowakutanisha Ureno dhidi ya Hispania.




WANAFUNZI MWISHO KUSOMEA KWENYE MIEMBE

Rais atangaza zoezi la ukaguzi wafanyakazi


Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ametangaza kuwa serikali yake iliyopo madarakani itafanya zoezi la ukaguzi wa aina ya maisha wanayoishi wafanyakazi wa umma.
Rais Kenyatta amesema wafanyakazi wote wa umma akiwemo yeye mwenyewe na Naibu wake William Ruto watatakiwa kutoa maelezo ya mali wanazomiliki na wale watakaobainika kuiba fedha za umma watawajibishwa kwa mujibu wa sheria.
Kauli ya Rais Kenyatta ameitoa wakati huu ambapo nchi hiyo ikishuhudia kampeni kubwa ya kupambana na vitendo vya rushwa ambapo hivi karibuni maofisa kadhaa wa serikali walikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya ubadhirifu wa mali za umma na matumizi mabaya ya ofisi.
Maafisa wa serikali na watu wengine zaidi ya 40 wameshtakiwa kwa wizi wa mamilioni ya Dola zilizokuwa zimetengewa kwa ajili Shirika la Huduma kwa Vijana NYS.

June 14, 2018

Marekani inaitaka Korea Kaskazini kuangamiza silaha za kivita

North Korea's leader Kim Jong Un is seen with an intercontinental ballistic rocket in this undated photo released by North Korea's Korean Central News Agency (KCNA) in Pyongyang 30 November 2017.



Marekani ina matumaini ya kuanza kuona shughuli ya kuangamizwa silaha nchini Korea Kaskazini ifikapo mwaka 2020, mwa mujibu wa waziri wa mashauri ya nchi za kigeni Mike Pompeo.
Matamshi yake aliyoyatoa alipofanya ziara nchini Korea Kusini, yanafuataia mkutano kati ya Rais Donald Trump na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un.
Walisaini makubaliano ya kufanya kazi katika kuangamiza kabisa silaha za nyuklia katika rasi ya Korea.
Lakini nakala hiyo imekosolewa kwa kukosa taarifa za kina kuhusu ni lini na ni vipi Korea Kaskazini itaachana na silaha zake.


US Secretary of State Mike Pompeo, right, arrives in Seoul, 13 June 2018Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMike Pompeo (kulia) akiwa Seol

Bw Pompeo alisafiri kutoka Singapore kwenda Seoul ambapo alikuwa akihifahamisha serikali ya Korea Kusini kuhusu matokeo ya mkutano huo.
Alsema bado kuna kazi nyingi ya kufanywa na Korea Kaskazini, "ya kuangamiza silaha ... Tuna matumaini kuwa tutaweza kutimiza hilo ndani ya miaka miwili unusu."
Alisema ana uhakika kuwa Pyongyag ilikuwa inafahamu kuwa shughuli yoyote ya kuangamiza programu yake za nyuklia itahitaji hakikisho.


US President Donald Trump disembarks from Air Force One upon arrival at Joint Base Andrews in Maryland on 13 June 2018Haki miliki ya pichaAFP
Image captionTrumop akiwasili nyumbani baada ya mkutano na Kim

Rais Trump mapema alitangaza kuwa Korea Kaskazini sio tena tisho la nyuklia akisisitiza kuwa kila mtu sasa anaweza kuhisi salama.

Kipi kiliafikiwa kwenye mkutano huo?

Viongozi hao walisema watashirikana katika kujenga uhusiano mpya huku Marekani ikiihakikishia usalama Korea Kaskazini.
Pyongyan nayo itajitolea katika kuangamzia silaha za nyuklia kwenye rasi ya Korea.
Kisha kwenye mkutano na waandishi wa habari Trump akasema kuwa ataiondolewa Korea Kaskazini vikwazo wakati suala la silaha za nyuklia litatatuliwa.


South Korean and US tanks fire live rounds during a joint live-fire military exercise near the demilitarized zone, separating the two Koreas in Pocheon, South Korea. April 21, 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMarekani hufanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi na Korea Kusini na pia Japan

Alisema anaamini kuwa Bw Kim atatekeleza yale ambayo ameyasema.
Alitangaza kusitishwa mazoezi ya kijeshi ambayo hufanyika mara kwa mara kati ya wanajeshi wa Marekani na Korea Kusini katika rasi wa Korea
Hatua hiyo imekuwa ikiitishwa kwa muda na Pyongyang na ilitangazwa bila matarajio kutoka kwa washirika wa Marekani na iliwapata kwa mshangao.
Makao rasmi ya rais wa Korea Kusini ya Blue House baadaye yalisema yalitaka kufahamu maana kamili ya matamshi ya Trump kuhusu kusitisha mazoezi ya kijeshia ya pamoja.

MUSSA NTIMIZI  KUJENGA TABORA MPYA 2018

Kombe la Dunia Urusi 2018: Urusi tayari kwa michuano mechi ya kwanza ikiwa Russia v Saudi Arabia


Image result for uwanja wa mpira wa miguu Urusi

Michuano ya Kombe la Dunia ya Fifa ya mwaka 2018 inaanza leo nchini Urusi ambapo Urusi watacheza dhidi ya Saudi Arabia baada ya kufanyika kwa sherehe ya ufunguzi katika uwanja wa Luzhniki, mjini Moscow.
Mechi hiyo itaanza saa kumi na mbili jioni saa za Afrika Mashariki.
Michuano hiyo itashirikisha mataifa 32, wakiwemo mabingwa watetezi Ujerumani, na itakuwa na mechi 64 zitakazochezwa katika kipindi cha siku 32.
Fainali itachezwa 15 Julai.
Fainali za sasa za Kombe la Dunia ambazo ni za 21 zitachezwa katika viwanja 12 katika miji 11 nchini Urusi, ambayo inapatikana eneo la upana wa maili zaidi 1,800.
Kutokana na hili, kutakuwa na tofauti kubwa katika wakati mechi zinachezwa.
Ujerumani, waliowashinda Argentina katika fainali ya Kombe la Dunia 2014, wanapania kuwa taifa la kwanza kushinda kombe hilo mtawalia kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1962.
Brazil nao wanatafuta kuweka rekodi nyingine kwa kushinda kombe hilo kwa mara ya sita.
Michuano hiyo ya mwezi mmoja inatarajiwa kuwavutia mashabiki nusu milioni kwenda Urusi na kote duniani inatarajiwa kutazamwa na watu zaidi ya bilioni tatu.
Kuna makundi manane, kila kundi likiwa na timu nne.
Timu mbili ambazo zitamaliza juu kwenye kundi ndizo zitakazosonga hadi hatua ya 16 bora.
Fainali itachezewa katika uwanja wa Luzhniki ambao hutoshea mashabiki 81,000 mnamo 15 Julai.

Nani atashinda Kombe la Dunia?

Mabingwa watetezi Ujerumani, mabingwa mara tano Brazil, washindi wa Euro 2016 Ureno, waliomaliza wa pili 2014 Argentina, Ubelgiji, Poland na washindi wa mwaka 1998 Ufaransa ni timu nane ambazo zilikuwa kwenye chungu wakati wa kufanywa kwa droo.
Wote wanapigiwa upatu kushinda.

Germany lifting the Fifa World CupHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionUjerumani ndio mabingwa watetezi

Wenyeji Urusi walikuwepo kwenye chungu pia ingawa ndio walioorodheshwa wa chini zaidi kwa viwango vya soka kwa kufuata orodha ya Fifa ya kila mwezi, ambapo kwa sasa wameorodheshwa wa 70.
England, ambao wameshinda mechi moja pekee kati ya nane walizocheza karibuni zaidi Kombe la Dunia hawakuwa kwenye chungu, sawa na mabingwa wa mwaka 2010 Uhispania.
Ujerumani wamefika angalau nusu fainali katika kila michuano minne iliyochezwa karibuni, na baada ya kuwa timu pekee kufuzu kwa kushinda mechi zote Ulaya, wanatarajiwa kutoa ushindani mkali.
Wamo Kundi F na Mexico, Sweden na Korea Kusini.
"Ujerumani watawindwa kama ambavyo haijawahi kutokea awali," anaamini kocha wao Joachim Low.
"Ni sisi pekee, kama mabingwa watetezi, tuna kitu cha kupoteza."
Brazil ndiyo nchi pekee ambayo imeshiriki michuano hiyo bila kukosa tangu ilipoanzishwa lakini hawajashinda tangu 2002.
Mara ya mwisho kwao kushinda wakiwa barani Ulaya ilikuwa ni mwaka 1958.

World CupHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES

Hata hivyo, Brazil wana matumaini, hasa kupitia nyota wao Neymar aliyeweka rekodi ya dunia kwa kununuliwa £200m alipohamia Paris Saint Germain ya Ufaransa kutoka Barcelona Agosti 2017.
Alikuwa ameumia mapema mwaka huu lakini amepona na kucheza mechi kadha za kirafiki za kimataifa akiwa na Brazil, na kufunga.
Uhispania wana mabingwa kadha wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kutoka Real Madrid kwenye kikosi chao na watatakakutwaa kombe hilo tena kama walivyofanya miaka minane iliyopita, na waliposhinda ubingwa Ulaya 2008 na 2012.

Ronaldo na Messi watafanikiwa?

Upande mwingine, Cristiano Ronaldo naye atakuwa anatafuta medali yake ya kwanza ya kushinda Kombe la Dunia baada ya kuwasaidia Ureno kushinda Euro 2016, Lionel Messi naye akitumai kwamba atashinda kombe lake la kwanza kuu akiwa na Argentina.
Ufaransa wana kikosi kichanga na kilichojaa wachezaji wa kusisimua, akiwemo mshambuliaji wa miaka 19 Kylian Mbappe.
Aidha, wana wachezaji nyota kutoka Ligi ya Premia wakiwemo kipa wa Tottenham Hugo Lloris, kiungo wa kati wa Manchester United Paul Pogba na mshambuliaji wa Chelsea Olivier Giroud.
Walio wageni Kombe la Dunia ni kina nani?
Panama na Iceland watakuwa wanashiriki Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza.
Iceland ambalo ni taifa la watu 335,000 pekee ndilo taifa ndogo zaidi linaloshiriki.
Watatumai watarudia ufanisi wao wa miaka miwili iliyopita walipofika robofainali Euro 2016 mara yao ya kwanza kushiriki michuano mikubwa. Walifanya hivyo kwa kuwaaibisha England njiani.
Mechi ya kwanza kwa Iceland nchini Urusi itakuwa dhidi ya Argentina 16 Juni.
Sikukuu ya taifa ilitangazwa Panama baada yao kufuzu kwa Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza.
Taifa hilo la Amerika ya Kati limeorodheshwa la 55 katika viwango vya soka vya Fifa. Wana mkufunzi mwenye uzoefu mkubwa Hernan Dario Gomez, aliyekuwa na taifa lake la Colombia Kombe la Dunia la 1998 na Ecuador mwaka 2002.
Kuna mataifa kadha pia ambayo yamerejea baada ya kuwa nje kwa muda mrefu.
Misri na Morocco wamerejea baada ya kutoshiriki kwa miaka 28 na 20 mtawalia.
Kuna mataifa yanayofahamika sana kwa soka ambayo hayashiriki.
Mabingwa mara nne Italia, mabingwa wa Amerika ya Kusini Chile na mabingwa wa Africa Cameroon wote hawakufanikiwa kufuzu.
Uholanzi, waliomaliza wa pili mwaka 2010 pia hawakufanikiwa.
Marekani nao wanakosa michuano hiyo kwa mara ya kwanza tangu 1986.
Waamuzi kusaidiwa na VAR
Teknolojia ya kuwasaidia waamuzi (VAR) itatumiwa kwa mara ya kwanza Kombe la Dunia wakati huu.
Teknolojia hiyo itatumiwa kuwasaidia waamuzi kuepuka makosa ambayo yanaweza kusaidia kuamua mshindi wa mechi, hasa wakati wa kukubali goli, mikwaju ya penalti au kadi nyekundu.
VAR tayari imekuwa ikijaribiwa England, Ujerumani na Italia.
Teknolojia hiyo ilitumiwa mara ya kwanza katika Kombe la Dunia la Klabu Desemba 2016 na ikajaribiwa katika Kombe la Mashirikisho 2017.

Fans will be able to watch every match broadcast by the BBC from the corporation's virtual reality sofa
Image captionBBC Idhaa ya Kiswahili itatangaza moja kwa moja mechi za michuano hiyo

Usalama

Urusi inapanga kuandaa michuano ya kufana baada ya kuwashinda England, Uhispania na Ureno, na Uholanzi na Ubelgiji, katika kupigania haki za kuwa mwenyeji.
Ni mara ya kwanza Urusi kuandaa michuano hiyo.
Mashabiki karibu 10,000 wa England wanatarajiwa kusafiri Urusi, lakini baadhi huenda wasisafiri kutokana na uhasama uliozidi kati ya nchi hizo mbili na wasiwasi pia kuhusu usalama.
Makabiliano yalitokea kati ya mashabiki wa Urusi na England mataifa hayo yalipokutana Marseille wakati wa Euro 2016.
Ghasia pia zilizuka kati ya mashabiki wa England, Urusi na Ufaransa.