August 31, 2018

Kituo cha sheria na haki LHRC: Watoto 394 hubakwa kila mwezi Tanzania


Watoto wakicheza
Ripoti iliyotolewa na kituo cha sheria na haki za binadamu nchini Tanzania imebainisha kwamba kuna ongezeko kubwa la ukatili dhidi ya watoto kwa kipindi cha miezi sita ya kwanza katika mwaka 2018.
Ongezeko kubwa la matukio ya ubakaji wa watoto ni mara tatu zaidi ikilinganishwa na kipindi cha mwaka 2017, kutoka 12 kwa mwaka hadi 533 kwa mwaka 2018.
Hivyo ni wastani wa watoto 394 wamebakwa kila mwezi katika maeneo mbalimbali ya Tanzania bara kuanzia mwezi Januari hadi Juni 2018

August 24, 2018

Mwanamke wa kwanza rubani wa ndege ya vita


Luteni Misa Matsushima.
Mwanamke mmoja nchini Japan amefuzu kuwa rubani wa kwanza wa ndege za kivita nchini humo, Luteni Misa Matsushima, mwenye umri wa miaka 26, ameanza majukumu yake leo baada ya kumaliza mafunzo ya kurusha ndege ya kivita aina ya F 15, jeshi la Japan limetangaza.


Luteni Misa amewaambia wanahabari kwamba, kwa kuwa rubani wa kwanza mwanamke atafungua fursa kwa wanawake wengine kuingia kwenye fani hiyo.
Tangu nilipoangalia sinema ya Top Gun, wakati nikiwa shule ya msingi basi nikatokea kuwapenda sana marubani wa ndege za kivita,” anasisitiza Misa.
Japan ina viwango vya juu vya ukosefu wa usawa wa kijinsia, ambapo wanawake wengi wanatarajiwa kuwa mama wa nyumbani badala ya kuajiriwa, lakini kutokana na kukabiliwa na changamoto ya kuwa na wazee wengi, mnamo mwaka 2013 Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Shinzo Abe, aliahidi kuwawezesha zaidi wanawake katika ajira.
Jeshi la Japan lilianza kuajiri wanawake kwa mara ya kwanza mwaka 1993 isipokuwa kwa marubani, ambapo iliondoa amrufuku hiyo mwaka 2015, ambapo kwa sasa wanawake wengine watatu wamejiunga kwenye mafunzo ya kuwa marubani wa ndege za kivita.

Mambo matano tunaweza kujifunza kutoka kwa sokwe kuhusu siasa


Chimpanzee with fingers in its ears
Kuna tofauti kati ya siasa zetu na zile za viumbe wengine waofanana na binadamu.
Profesa James Tilley amekuwa akifanyia utafiti kile tunaweza kujufunza kisiasa kutoka kwa mivutano ya mamlaka kutoka kwa makundi ya sokwe.

1. Kuwa na uhusiano wa karibu na marafiki lakini pia maadui wawe karibu zaidi

Two chimpanzees, sitting on sand,Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKuwa na uhusiano wa karibu na marafiki lakini pia maadui wawe karibu zaidi
Siasa za sokwe ni miungano inayozidi kubadilika na ikiwa utahitaji kubakia madarakani unahitaji kuwa tayari kuwageuka marafiki na kuwaenzi maadui.

2. Wakati wa kujenga miungano chagua mtu dhaifu badala ya yule aliye na nguvu

Two smiling chimpanzees sitting on a tree with arms crossedHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionWakati wa kujenga miungano chagua mtu dhaifu badala ya yule aliye na nguvu
Sokwe hupanda kuwa na miungano dhaifu.
Hii inamaanisha kuwa sokwe wawili dhaifu watamuunga mkono sokwe mmoja mwenye nguvu.
Ikiwa tutafikiria hivyo basi inaweza kuwa na manufaa.

3. Ni vizuri uogopwe lakini pia ni vizuri zaidi upendwe.

Chimpanzees sitting on a rockHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionNi vizuri kuwa maaarufu kwenye siasa
Viongozi wa sokwe huogopwa sana na hutawala kwa nguvu, lakini viongozi hawakai siku nyingi.
Kuwa kiongozi mwenye kufanikiwa ni lazima utafute uungwaji mkono kutoka kwa wengi na kuwa mkarimu ndio suluhu.

4. Ni vizuri kupendwa, lakini pia ni vizuri zaidi kutoa vitu kama zawadi

Three chimpanzees sit in a group appearing to have a meetingHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionChukua hii rafiki yangu
Viongozi wanaotawala kwa muda mrefu ni wale huchukua mali na kuitumia mali hiyo kununua uungwaji mkono.

5. Vitisho vya nje vinaweza kuchangia uungwaji mkono (ikiwa ni vya kweli...)

Chimpanzee family is sitting in a treeHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionWakati kuna vitisho vya kutoka nje, makundu ya sokwe huja pamoja na kupambana kwa pamoja.
Wakati kuna vitisho vya kutoka nje, makundu ya sokwe huja pamoja na kupambana kwa pamoja.
Isipokuwa hili hufanyika tu kwa binadamu kama kuna tisho lisilotarajiwa kama mashambulizi ya 9/11

DIWANI WA CHADEMA AHAMIA CCM BAADA YA KUVUTIWA NA DREAMLINER



Uamuzi mgumu wa Rais John Magufuli wa kuboresha usafiri wa anga nchini kwa kununua ndege kubwa ya Boeing 787-8 Dreamliner, umemkimbiza Diwani wa Chadema katika kata ya Ndumeti, Wilaya ya Siha, Jackson Rabo kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Kwa mujibu wa diwani huyo moja ya sababu iliyomvutia kujiunga na CCM baada ya uamuzi wa Rais John Magufuli kuhamishia ofisi zote za serikali mkoani Dodoma.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Valerian Juwal amethibitisha kuwa Diwani Jackson Rabo anakuwa Diwani wa tano katika wilaya hiyo kujiuzulu mwaka huu.

Beyonce and Jay Z presented the Key to the city of Columbia



Columbi Mayor Steve Benjamin has presented the Key to the city of Columbia to Beyoncé and JAY-Z for their humanitarian and cultural contribution to the city.
The presentation followed their thrilling OTR II performance at Williams – Brice stadium.
Confirming the news, Steve Benjamin shared via Twitter:
”Late night but what an incredible show at #OTRII in @ColumbiaSC ! It was wonderful to have a chance to recognize the humanitarian & cultural contributions of Mr. & Mrs. Carter. August 21st was officially “Beyoncé Knowles Carter & Shawn Carter Day” in @ColumbiaSC @Beyonce @SC

August 21, 2018

IJUE EBOLA ,DALILI ZAKE,MAAMBUKIZI NA NJIA ZA KUJIKINGA



images (1)
images (2)
EBOLA ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambavyo uishi katika miili ya binadamu na wanyama. Kwa mara ya kwanza ugonjwa huu ulitokea mwaka 1972  katika milipuko miwili iliyotokea kwa pamoja katika sehemu ya Nzara nchini Sudan na Yambuku nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo karibu na mto Ebola ambapo jina la ugonjwa huu lilipatikana. Toka kipindi hicho kumekuwa na muendelezo wa milipuko mbalimbali katika nchi tofauti za Afrika katika miaka tofautitofauti.
Mlipuko wa sasa wa ugonjwa wa Ebola umetokea katika nchi zilizopo magharibi mwa Afrika ,kesi ya kwanza iligunduliwa mwezi Machi,2014. Mlipuko wa sasa ni mkubwa zaidi kuwahi kutokea toka virusi wasababishao ugonjwa huu ulipogunduliwa mwaka 1976 ukiwa umesababisha vifo vingi zaidi kuliko milipuko yote ya miaka ya nyuma kwa pamoja.Mlipuko wa sasa umeathiri nchi nyingi zaidi,miongoni mwa nchi zilizoathrika sana ni Guinnea,Sierra Leone na Liberia.Kutokana na mlipuko wa sasa kuwa na athari kubwa na kuathiri nchi Zaidi mnamo Agusti 8,2014 shirika la afya ulimwenguni (WHO) lilitanganza mlipuko huu kuwa ni dharura ambayo nchi zote duniani zilitakiwa zishiriki katika harakati za kuudhibiti.
DALILI ZA UGONJWA WA EBOLA
Dalili za ugonjwa wa Ebola huaanza kuoneekana siku 2 mpaka 5 tangu mtu apate maambukizi ila kwa wastani ni siku 8 mpaka 10.
Zifuatazo ni dalili kuu za ugonjwa wa Ebola;
  • Homa
  • Maumivu makali ya kichwa
  • Maumivu ya misuli
  • Kufa ganzi
  • Kuharisha
  • Kutapika
  • Maumivu ya tumbo
  • Kutokwa damu pasipo sababu sehemu mbalimbali za mwili
Unapoona dalili moja au zaidi kati ya hizi unatakiwa uwahi mara moja katika kituo cha afya kwa uchunguzi Zaidi na matibabu itakapohitajika.
NJIA ZA MAAMBUKIZI YA EBOLA
  • Ugonjwa wa Ebola usambazwa kwa njia ya kugusa majimaji ya mwili wa mgonjwa au mnyama aliyeathiriwa na ugonjwa huu. Majimaji yatokanayo na damu,kinyesi na matapishi yanasababisha maambukizi kwa kiasi kikubwa.
  • Virusi vya Ebola pia hupatikana katika maziwa ya mama,mkojo na shahawa.Virusi huendelea kupatikana kwa siku 70 hadi 90 kwenye shahawa za mwanaumme aliye na ugonjwa huu.
  • Machozi na mate pia yanaweza kuwa na virusi vya ugonjwa huu
  • Virusi vya Ebola pia vinaweza kusambazwa kwa njia ya kugusa sehemu na vitu kama meza,vitinda na kadhalika ambavyo vina virusi tayari.
  • Virusi vya Ebola mara nyingi havisambazwi kwa njia ya hewa ila vinaweza kusambaa kwa njia ya matone ya majimaji yanayotoka kinywani au puani pale mgonjwa anapokohoa au kupiga cha fya.
NJIA ZA KUJIKINGA NA EBOLA
  • Hakikisha usafi wa mwili wako, kwa mfano osha mikono yako kwa maji safi na sabuni na epuka kugusa damu au majimaji ya mtu yeyote.
  • Usiguse vitu kama nguo,shuka,vifaa vya matibabu na kadhalika ambavyo vimeguswa na damu au majimaji ya mgonjwa wa Ebola
  • Epuka kushiriki mazishi ambayo yanahusisha kugusa mwili wa mtu aliyefariki.
  • Epuka kugusana na popo na wanyama jamii ya sokwe au majimaji,damu na nyama zao .
  • Epuka kusogelea sehemu zilizotengwa kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa wa Ebola
  • Baada ya kutoka eneo lenye mlipuko wa ugonjwa huu fuatilia kwa umakini afya yako kwa kipindi cha siku 21 na ukiona dalili zozote za ugonjwa huu nenda kituo cha afya mara moja.
NJIA ZA KUJIKINGA KWA WATOA HUDUMA ZA AFYA
Wahudumu wa afya ni miongoni mwa watu walio katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya ugonjwa huu kutokana na ukaribu walionao na wagonjwa.Kutokana na hali hiyo Wahudumu wa afya wanatakiwa kuwa makini sana wanapotoa huduma kwa wagonjwa.
  • Vaa nguo zinazotakiwa za kujikinga na maambukizi
  • Tenga wagonjwa wa Ebola na wagonjwa wengine
  • Epuka kugusa moja kwa moja bila kinga miili ya watu waliofariki kutokana na Ebola
  • Ikitokea umegusa moja kwa moja majimaji,damu,mkojo,machozi au shahawa za mgonjwa wa Ebola toa taarifa haraka kwa afisa wa afya.




August 16, 2018

Rais Mstaafu akataa kuchukua malipo yake ya uzeeni



Aliyekua rais wa Uruguay Jose Mujica, aliyejulikana kama rais maskini zaidi duniani amesema hatachukua malipo yake ya uzeeni tangu aanze kuhudumu kama seneta.

Mujica aliacha kazi ya useneta mnano Jumanne, kiti ambacho amekua akishikilia tangu muda wake wa kuhudumua kama raisi ukamilika mwaka wa 2015.

Alidai kuwa amechoka na hangeweza kuendelea na kazi hadi mwaka wa 2020. Muasi huyo wa zamani wa mrengo wa kushoto ana miaka 83.

Mujica aliwasilisha barua ya kuacha kazi kwa mkuu wa seneti. Alisema ya kwamba fikra ya kuacha kazi ni ya kibinasfi huku akiongeza kuwa ni uchovu wa safari ndefu.

Hata hivyo aliongeza kua ataendelea kuchangia hoja kwa sababu bado akili yake inafanya inafanya kazi.

Mujica anayejulikana kwa matamshi yake ya kichesi aliomba msamaha kwa wenzake kwa uamuzi huo.

Mwaka 2016, alidai rais wa Venezuela Nicolás Maduro ni mwendazimu kama mbuzi.

Umaarufu wake ulienea kutokana na maisha yake ya chini ya kukataa kuishi kwenye ikulu ya rais.

August 14, 2018

Komu afunguka kutimkia CCM


Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini (CHADEMA), Anthony Komu.
Akizungumza na East Africa BreakFast ya East Africa Radio amesema kuwa hawezi kuondoka CHADEMA na hajawahi kufanya mazungumzo na Waitara kuhusu suala hilo kwani yeye ndio muasisi wa upinzani na anajivunia historia hiyo .
Mimi sio sehemu ya mpango huo na sielewi Waitara katoa wapi taarifa hiyo naomba wananchi wangu watambue kuwa mimi sio mpinzani wa kuunga unga mimi ni miongoni mwa waasisi wa upinzani”, amesema Komu.
Jumamosi ya Agosti 11, 2018 kupitia Weekend BreakFast ya East Africa Radio Waitara aliwataja wabunge watano kutoka CHADEMA wanaotaraji kujiunga na CCM akiwemo Anthony Komu.
Msikilize hapo chini Komu amefunguka zaidi.

Meli ya mizigo yawaka moto bandari ya Bagamoyo


Mfano wa picha ikionesha Meli ikiwaka moto.
Meli ya mizigo ijulikanayo kama LCT Rahimu imewaka moto mapema leo ikiwa katika bandari ya Bagamoyo.

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo, Fatuma Latu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kutaja chanzo chake kuwa ni hitilafu ya umeme wakati mafundi wakijaribu kuchomelea mlango wa meli hiyo kwa kutumia umeme wa jenereta iliyokuwa ndani yake.
Amesema vyombo vya zimamoto na uokoaji vimefanikiwa kuzima moto huo na kwamba nahodha kwa sasa anahojiwa na vyombo vya usalama ili kupata maelezo zaidi.
Inadaiwa kuwa meli hiyo imetokea visiwani Zanzibar na ilikuwa bandarini hapo ikisubiri shehena ya kokoto kwa ajili ya kuipeleka Zanzibar.

Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 14.08.2018

Christian Eriksen
Paris St-Germain wanaandaa pauni milioni 100 kwa ofa ya mchezaji wa Tottenham mwenye miaka 26 raia wa Denmark Christian Eriksen. (Express)
Schalke wana nia ya kumasaini mchezaji mwenye miaka 22 raia wa England Reuben Loftus-Cheek kwa mkopo lakini Chelsea haunda wasiruhusu kuondoka kwake. (Telegraph)
Matteo DarmianHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMatteo Darmian
Beki wa Manchester United Matteo Darmian anataka kuondoka Old Trafford na Juventus, Napoli na Internazionale wanamwinda mchezaji huyo mwenye miaka 28 raia wa Italia. (Manchester Evening News)
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho aliachanganyikiwa kufuatia madai ya Paul Pogba ya kuwepo uhusiano mbaya kati yao siku ya Ijumaa. (Telegraph)
Marcus BettinelliHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMarcus Bettinelli
Kipa Marcus Bettinelli, 26, anaweza akaamua kuondoka Fulham baada ya kuachwa nje ya kikosi kilichocheza mechi ya kwanza ya msimu. (Mail)
Liverpool watasikiliza ofa kwa mchezaji wa maiaka 32 mlinzi rauia wa Estonia Ragnar Klavan. (Liverpool Echo)
Lee CattermoleHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionLee Cattermole
Kiungo wa kati wa Sunderland mwenye miaka 30 Lee Cattermole huenda akahamia Bordeaux, ambapo aliyekuwa meneja wa zamani wa Black Cats sasa ndiye meneja. (Teamtalk)
Wale wanaolengwa kuchukua nafasi ya mkurugenzi mpya wa Manchester United ni pamoja na kipa Edwin van der Sar, mkurugenzi wa Juventus Fabio Paratici na Monchi, mkurugenzi wa zamaniawa Sevilla na sasa Roma. (Independent)
Wilfried ZahaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionWilfried Zaha
Mshambuliaji Wilfried Zaha anasema bado anazungumza na Crystal Palace kuhusu kuongezwa mkataba wake huko Selhurst Park. (Mail)
Meneja wa zamani wa Argentina Jorge Sampaoli anataka kurudi kwenye usimamizi na Mexico. (Goal)
Paris St-Germain na Monaco wanataka kiungo wa kati wa Sevilla mwenye miaka 29 Mfaransa Steven Nzonzi. (France Football)
Maxim Choupo-MotingHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMaxim Choupo-Moting
Kiungo wa kati mwenye miaka 25 Giannelli Imbula, kiungo wa kati mwenye miaka 32 msikochi Charlie Adam, winga raia wa Cameroon mwenye miaka 29 Maxim Choupo-Moting na mlinzi mwenye miaka 33 Geoff Cameron wote wana mpango wa kuondoka Stoke. (Telegraph)
Meneja wa Real Madrid Julen Lopetegui anataka kuongeza mlinzi na mshambuliaji kwenye kikosi chake kabla ya tarehe ya mwisho. (AS)
Julen Lopetegui aHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionJulen Lopetegui a

Bora zaidi kutoka Jumatatu

AC Milan wanamtafuta kiungo wa kati wa Chelsea mwenye miaka 23 Tiemoue Bakayoko kwa mkopo wa msimu wote kabla ya kumpa mkataba wa kudumu. (Sun)
Tiemoue BakayokoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionTiemoue Bakayoko
Barcelona itamwinda Paul Pogba baada ya msimu wa joto wa kununua wachezaji kukamilika tarehe 31 Agosti kufuatia kukubali kuwa Manchester United hawatamuuaza mchezaji huyo mwenye miaka 25 raia wa Ufarasa mwezi huu. (Telegraph)
Kipa wa Liverpool Loris Karius, 25, anawindwa na Besiktas. Klabu hiyo wa Uturuki imekuwa na mpango wa kumsaini Mjerumani huyo kwa mkopo wa msimu wote. (Sun)
Loris KariusHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionLoris Karius
Beki wa Manchester City mwenye miaka 23 Jason Denayer amekataa kuondoka kwa mkopo kwa kuwa mchezaji huyo wa kimataifa raia wa Ubelgiji anataka kuhamia klabu ya Uturuki ya Galatasaray. (Star)
Cristiano Ronaldo amewashauri Juventus kumuendea kiungo wa kati wa Lazio Sergej Milinkovic-Savic. Mchezaji huyo mwenye miaka 23 raia wa Serbia amehusishwa na Manchester United na Chelsea. (Star)
Cristiano RonaldoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionCristiano Ronaldo
Kiungo wa kati wa Paris St-Germain Adrina Rabiot, 23, amekataa ofa ya kusaini upya mkataka wake na mabingwa hao wa Ligue 1. Mkataba wa kwanza wa Mfaransa huyo unakamilika mwisho wa msimu. (L'Equipe)