Header Ads

China na Korea Kaskazini zafanya mazungumzo

Kiongozi wa China akutana na mwenzake wa Korea Kaskazini


Kitengo cha taifa cha habari nchini Korea Kaskazini kimeripoti kwamba mjumbe maalum wa China Song Tao amefanya mazungumzo na Choe Ryong-Hae , ambaye ni mshauri wa karibu wa rais wa Korea Kaskazini Kim Jong un .
Ziara hiyo ambayo ni ya kwanza kuwahi kufanywa na afisa mwanadimizi wa China katika kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja inajiri wakati ambapo kuna hali ya wasiwasi mwingi kati ya washirika hao wawili na inafuatia ziara ya rais Trump katika eneo hilo.
Trump amekuwa akiishinikiza China kuiwekea vikwazo vya Umoja wa mataifa Korea Kaskazini
China haijatoa maelezo ya ziara hiyo, lakini vyombo vya habari vya Korea Kaskazini vimesema kwamba bwana Song alisisitiza kuhusu mpango wa Bejing wa kuimarisha urafiki wa miaka mingi uliokuwepo kati ya mataifa hayo mawili.

No comments