Header Ads

Duterte aahidi polisi waliomuua kijana wa miaka 17 watakwenda jela



Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte, jana ameuhakikishia umma wake kwamba maafisa wa polisi waliohusika na kifo cha kijana wa kiume aliyekuwa na umri wa miaka 17 wakati wa operesheni ya kupambana na madawa ya kulevya watatumikia kifungo jela, 

wakikutikana na hatia. Duterte ameongeza kwamba Idara ya Sheria tayari imeshaiamuru Ofisi ya Taifa ya Uchunguzi kubaini iwapo maafisa wa polisi walihusika katika kifo cha, Kian Loyd Delos Santos, kilichotokea wiki iliyopita. Masaa machache kabla ya hapo, 

mamia ya watu waliandamana katika mji mkuu wa Manila, kupinga kifo cha Delos Santos, ambaye familia yake na marafiki wamekana kwamba alikuwa mtumiaji wa madawa ya kulevya. Kampeni ya kupambana na madawa ya kulevya ya Rais Duterte, ambayo imesababisha vifo vya maelfu ya watu ndani ya mwaka mmoja, imekuwa ikishutumiwa sana na makundi ya kutetea haki za binaadamu pamoja na serikali za kigeni.

No comments