Header Ads

Marekani na Korea Kusini zaanza mazoezi ya kijeshi



Südkorea Gemeinsame Militärübung mit der USA (Getty Images/AFP/Jung Yeon-Je)

Wanajeshi wa Marekani na Korea Kusini wameanza mazoezi ya kijeshi ya kila mwaka, baada ya marais wa Marekani na Korea Kaskazini kujibizana maneno ya kuashiria vita na majaribio mawili ya makombora ya Korea Kaskazini.
Mazoezi hayo ya pamoja ya kijeshi ya kila mwaka yajulikanayo kama 'Ulchi Freedom Guardian' ambayo kwa kiasi kikubwa yanaendeshwa kwa kompyuta kwa teknolojia ya kidijitali na kufanyika kila majira ya joto, yamepokewa kwa hasira na upande wa Korea Kaskazini, ambayo inayatazama kama mazoezi ya kujitayarisha kwa uvamizi.

Akizungumza na Baraza lake la mawaziri, Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in, amesema leo  kwamba ushirikiano wa kijeshi kati ya Korea Kusini na Marekani haukusudii kuongeza mvutano kwenye rasi ya Korea, na ameionya Korea Kaskazini dhidi ya kulitumia zoezi hilo la kijeshi kama sababu ya kufanya vitendo vya uchochezi.
"Korea Kaskazini inapaswa kufahamu kwamba kutokana na uchokozi wake wa mara kwa mara, zoezi la pamoja kati ya Korea Kusini na Marekani litaendelea. Natumai kuwa maafisa wa serikali zetu pamoja na wanajeshi wapo tayari kujibu uchokozi wowote ule utakaotokana na zoezi la mara hii, na nawataka watu wetu kuwa na mshikamano zaidi kuliko wakati mwengine wowote," amesema Rais, Moon Jae-in, wa Korea Kusini.

No comments