Header Ads

Matukio ya Kisiasa Merkel asikitishwa na viwanda vya magari Kansela Angela Merkel alijibu maswali ya wapiga kura katika kipindi cha maswali na majibu cha televisheni, ambapo aliulizwa kuhusu usalama, wahamiaji na kashfa ya kupima moshi unaochafua mazingira kwa magari ya VW Deutschland Merkel Statement zum Barcelona Anschlag (picture-alliance/dpa/M. Kappeler) Kansela wa Ujerumani Angela Merkel Kampeni kuelekea uchaguzi mkuu wa Ujerumani mwezi ujao inaendelea. Bibi Markel Anagombea muhula wa nne. Kansela Angela Merkel alishiriki katika kipindi cha televisheni cha kituo cha RTL ambacho kilikuwa kinarushwa moja kwa moja, Jumamosi jioni. Wapiga kura walimuuliza maswali kansela wakati akiwania muhula wa nne madarakani katika uchaguzi wa mwezi Septemba. USA - Merkel als Malerei: The Art of Leadership in Dallas (picture-alliance/dpa/L. W. Smith) Picha ya kuchora ya kansela wa Ujerumani Angela Merkel Uchunguzi wa maoni ya wapiga kura unaonesha chama cha kansela Merkel cha Christian Democratic Unioni CDU pamoja na chama ndugu cha jimbo la Bavaria Christian Social Union , CSU vitakuwa kundi kubwa la chama bungeni lakini bila ya wingi wa kutosha. Kutokana na mashambulizi nchini Ujerumani na hivi karibuni kabisa mjini Barcelona, Merkel aliulizwa hatua gani serikali yake itachukua kuimarisha usalama. Merkel alisema kwamba mchanganyiko wa matumizi ya polisi na matumizi ya teknolojia inapaswa kutumiwa kuhakikisha usalama. Amesema kwamba wakati kuna raia wanaokadiriwa kufikia 10,000 ambao wamepata itikadi kali na kuwa na mawazo ya itikadi kali nchini Ujerumani, ni watu 600 hadi 700 tu wanaonekana kuwa ni hatari. Merkel amekosoa matumizi ya Uturuki ya jeshi la polisi wa kimataifa Interpol kumkamata kwa kutoa waranti na kutaka arejeshwe nchini humo mwandishi Mjerumani Dogan Akhanli kutoka nchini Uhispania siku ya Jumatatu kuwa na matumizi mabaya ya shirika hilo la polisi la kimataifa. "Sio sahihi na nafurahi sana kwamba uhispania imemuachia huru," Merkel amesema. "Hatupaswi kutumia vibaya mashirika ya kimataifa kama Interpol kwa madhumini hayo." Deutschland Bundeskanzlerin Angela Merkel im ARD-Interview (picture-alliance/dpa/R. Jensen) Kansela Angela Merkel akifanyiwa mahojiano na waandishi habari Kansela achukizwa na viwanda vya magari Kansela amesema atajaribu kuunganisha vifaa vya polisi na utaratibu wa majimbo 16 nchini Ujerumani. Amedokeza kwamba wengi hawafahamu upekuzi wa polisi pamoja na uangalizi wa vidio kwamba unafanyakazi kwa njia tofauti katika majimbo hayo nchini Ujerumani. Amesema chama chake cha Christian Democratic , kitajaribu kuunganisha mbinu za polisi , akisema : "Pia nitazungumza tena na mawaziri wakuu wa majimbo binafsi." Merkel pia alitetea uamuzi wake wa kufungua mipaka ya Ujerumani kwa mamia kwa maelfu ya wakimbizi miaka miwili iliyopita. Alipoulizwa iwapo sasa angefanya tofauti , alisema: "Bado nafikiri uamuzi wangu ulikuwa sahihi." Ametoa wito wa umoja zaidi katika bara la Ulaya kusaidia nchi kama Italia na Ugiriki kupambana na idadi kubwa ya wahamiaji wanaowasili katika mipaka yao. Merkel bei CDA Veranstaltung in Dortmund (picture-alliance/dpa/I.Fassbender) Bibi Angela Merkel Mpiga kura mmoja aliuliza swali kwamba kwanini waombaji hifadhi hawaruhusiwi kufanyakazi wakati kesi zao zikifanyiwa mapitio wakati baadhi wakisema wamesubiri kwa miaka kadhaa wakipiewa fedha za walipa kodi wakati wanataka kufanyakazi. Merkel amewaambia wapiga kura kwamba amevunjwa moyo na tasnia ya makampuni ya kutengeneza magari kufuatia kashfa ya dizeli ya kampuni ya Vilkswagen. Amesema waziri wa zamani wa mazingira alifahamu madhara yake. "Nimekasirishwa," Merkel amewaambia watazamaji. Tasnia ya magari imetishia kujiingiza katika matatizo makubwa katika kashfa hiyo na makampuni yanapaswa kujisahihisha kwa kiasi kikubwa kadri wanavyoweza," amedokeza. Amesema program mpya ipo kwa sasa kuweza kusahihisha makosa hayo. Mwandishi : Jane Mcintosh / ZR / Sekione Kitojo Mhariri: Mohammed Abrul Rahman



Merkel asikitishwa na viwanda vya magari 

 Deutschland Bundeskanzlerin Angela Merkel im ARD-Interview (picture-alliance/dpa/R. Jensen)

Kansela Angela Merkel alijibu maswali ya wapiga kura katika kipindi cha maswali na majibu cha televisheni, ambapo aliulizwa kuhusu usalama, wahamiaji na kashfa ya kupima moshi unaochafua mazingira kwa magari ya VW
Deutschland Merkel Statement zum Barcelona Anschlag (picture-alliance/dpa/M. Kappeler) Kansela wa Ujerumani Angela Merkel
Kampeni kuelekea uchaguzi mkuu wa Ujerumani mwezi ujao inaendelea.  Bibi Markel Anagombea  muhula  wa  nne. 
Kansela  Angela  Merkel  alishiriki  katika  kipindi  cha televisheni cha  kituo  cha  RTL ambacho  kilikuwa  kinarushwa  moja  kwa moja, Jumamosi  jioni. Wapiga  kura  walimuuliza  maswali  kansela wakati  akiwania  muhula  wa  nne  madarakani  katika  uchaguzi  wa mwezi  Septemba.

USA - Merkel als Malerei: The Art of Leadership in Dallas (picture-alliance/dpa/L. W. Smith) Picha ya kuchora ya kansela wa Ujerumani Angela Merkel
Uchunguzi  wa  maoni  ya  wapiga  kura  unaonesha  chama  cha kansela  Merkel  cha  Christian Democratic  Unioni  CDU  pamoja  na chama  ndugu  cha  jimbo  la  Bavaria  Christian Social  Union , CSU vitakuwa  kundi  kubwa  la  chama  bungeni  lakini  bila  ya  wingi  wa kutosha. Kutokana  na  mashambulizi nchini  Ujerumani  na  hivi karibuni  kabisa  mjini  Barcelona, Merkel  aliulizwa  hatua  gani serikali  yake  itachukua  kuimarisha  usalama.
Merkel  alisema  kwamba  mchanganyiko  wa  matumizi  ya  polisi  na matumizi  ya  teknolojia  inapaswa  kutumiwa  kuhakikisha  usalama. Amesema  kwamba  wakati  kuna  raia  wanaokadiriwa  kufikia 10,000   ambao  wamepata  itikadi  kali  na  kuwa  na  mawazo  ya itikadi  kali  nchini  Ujerumani, ni  watu 600  hadi  700  tu wanaonekana  kuwa  ni  hatari.
Merkel  amekosoa  matumizi  ya  Uturuki  ya  jeshi  la  polisi  wa kimataifa  Interpol kumkamata  kwa  kutoa  waranti  na  kutaka arejeshwe  nchini  humo mwandishi Mjerumani  Dogan Akhanli kutoka  nchini  Uhispania  siku  ya  Jumatatu  kuwa  na matumizi mabaya  ya  shirika  hilo  la  polisi  la  kimataifa. "Sio sahihi  na nafurahi  sana  kwamba  uhispania  imemuachia  huru," Merkel amesema. "Hatupaswi  kutumia  vibaya  mashirika  ya  kimataifa kama  Interpol kwa  madhumini  hayo."
Kansela Angela Merkel akifanyiwa mahojiano na waandishi habari
Kansela achukizwa na  viwanda vya magari
Kansela  amesema  atajaribu  kuunganisha  vifaa  vya  polisi  na utaratibu  wa  majimbo  16  nchini  Ujerumani. Amedokeza  kwamba wengi  hawafahamu upekuzi  wa  polisi  pamoja  na  uangalizi  wa vidio kwamba  unafanyakazi  kwa  njia  tofauti  katika  majimbo  hayo nchini  Ujerumani.
Amesema  chama  chake  cha  Christian Democratic , kitajaribu kuunganisha  mbinu  za  polisi , akisema : "Pia  nitazungumza tena na  mawaziri  wakuu  wa  majimbo  binafsi."
Merkel  pia  alitetea  uamuzi  wake  wa  kufungua  mipaka  ya Ujerumani  kwa  mamia  kwa  maelfu ya  wakimbizi miaka  miwili iliyopita. Alipoulizwa  iwapo  sasa  angefanya  tofauti , alisema: "Bado  nafikiri uamuzi  wangu  ulikuwa  sahihi." Ametoa  wito  wa umoja  zaidi  katika  bara  la  Ulaya  kusaidia  nchi  kama  Italia  na Ugiriki  kupambana  na  idadi  kubwa  ya  wahamiaji  wanaowasili katika  mipaka  yao.
Mpiga  kura  mmoja  aliuliza  swali  kwamba  kwanini  waombaji hifadhi  hawaruhusiwi  kufanyakazi  wakati  kesi  zao  zikifanyiwa mapitio  wakati  baadhi  wakisema  wamesubiri kwa  miaka  kadhaa wakipiewa  fedha  za  walipa  kodi wakati  wanataka  kufanyakazi.
Merkel  amewaambia  wapiga  kura  kwamba  amevunjwa  moyo  na tasnia  ya  makampuni  ya  kutengeneza  magari  kufuatia  kashfa  ya dizeli  ya  kampuni  ya  Vilkswagen. Amesema  waziri  wa  zamani wa  mazingira  alifahamu  madhara  yake. "Nimekasirishwa," Merkel amewaambia  watazamaji. Tasnia  ya  magari  imetishia  kujiingiza katika  matatizo  makubwa   katika  kashfa  hiyo na  makampuni yanapaswa  kujisahihisha  kwa  kiasi  kikubwa kadri wanavyoweza," amedokeza. Amesema  program mpya ipo  kwa  sasa  kuweza kusahihisha  makosa  hayo.
Mwandishi : Jane Mcintosh / ZR / Sekione  Kitojo
Mhariri: Mohammed Abrul Rahman

No comments