Header Ads

Polisi yamuua mshambuliaji wa Barcelona Younes Abouyaaqoub




Polisi wa Uhispania wa jimbo la Catalonia wamemuua kwa kumpiga risasi Younes Abouyaqoub, dereva anayeshukiwa kuendesha gari lililokanyaga watu katika shambulio la kigaidi la Barcelona. Abouyaqoub alipigwa risasi na kuuwawa kilomita 50 kutoka katika mji wa Barcelona siku nne baada ya kutokea shambulio hilo la kigaidi. Maafisa wamesema Abouyaqoub, ambaye ni raia wa Morocco aliyekuwa na umri wa miaka 22, aliendesha gari hilo na kuvamia kundi wa wapita njia katikati ya mji mkuu wa Barcelona wiki iliyopita, na kusababisha vifo vya watu 13 na kujeruhi wengine zaidi ya mia moja. Shambulio sawa na hilo lilitokea katika mji wa Cambrils, ambapo mwanamke mmoja alipoteza maisha kutokana na majeraha ya kuchomwa kisu. Kundi linalojiita Dola la Kiislam - IS limedai kuhusika na mashambulizi yote mawili.

No comments