Header Ads

JE? UNAJUA SABABU ZA KUACHWA NA MPENZI WAKO ?


Image result for JUA SABABU ZA KUACHWA
Add caption




Tujua ni rahisi kuamini wanawake wote ni vichaa, hawakuelewi, hawajui kipi wanahitaji na mengine mengi!". 

Tunaweza sema pole kwa bahati mbaya ulionayo, iwapo kama bahati ingekua kweli ndo inasababisha wewe kuachwa kwa kila uhusiano unaokuanao, tukiendana na ukweli kabisa, sababu ipo kwa yule unaemwangalia kwenye kiio kila mara ujiangaliapo, haiwezekani wewe kuwa unaachwa kwenye kila uhusiano unaokuanao na kusema sababu sio wewe.
Sio kusema kuwa wewe ni mtu mbaya au una sura ngumu kushinda wengine, hapana!, ila unakua unarudia kufanya maamuzi mabaya pamoja na kuwa na tabia flani flani mbaya ambazo zinasababisha haya kwa kila uhusiano unao ufanya na wewe kujikuta ukiachwa, kuna baadhi ya makosa kwenye uhusiano unajikuta unafanya bila ya wewe kujua.
Kama unataka kujua kwanini kuachwa ni kitendo kinachokua kinakutokea kwenye kila uhusiano, soma hapa na uone kama haya mambo ni mapya kwako..



1. Unamuhitaji mpenzi wako kupita kiasi.
    Hali ya kumuhitaji mpenzi wako ni kitu cha kawaida katika mahusiano, na ni hali ya kupendeza sana, ila hio hali ikivuka mipaka ni mbaya sana, inawezekana inatokana na shauku ya kuwa nae au hali ya wewe kutojiamani, na unakuwa tegemezi sana kihisia, usipomuona unakua kama unaumwa, na ukimwona kila saa unataka kuwa nae, hii inampa presha kubwa mpenzi wako kiasi mpaka anakuona kama mzigo na inashusha hamasa ya mapenzi kwake, hata mapenzi yanaitaji nafasi, na inawezekana ndo kisa cha kuachwa kwenye uhusiani uliopita, bila wewe kujua na kwenye uhusiano huu ndo unaongeza juhudi zaidi bila kujua ndo unaharibu zaidi.

    2. Una wivu unaopitiliza.
    Kuwa na wivu kidigo kwenye mapenzi ndo chachu ya mahusiano, ila kuanzisha ugomvi kila saa unapokuta amesimama na mwanaume ni mbaya, kama mpenzi wako anakushitumu kuwa na wivu wa kupitiliza unao mkera ujue uhusiano huo unaelekea pabayam na hamasa ya mapenzi kwa mpenzi wako itaanza kushuka. Kwanza hapo inamaanisha unatatizo la kutomwamini, ambalo inawezekana limesababishwa na uhusiano wa nyuma kabla ya huu ulionao, kwa mfano kama ulishawahi kufumania kwenye uhusiano uliopita au hujiamini kama mpenzi ulionae anakupenda kwa dhati!, na ni chanzo kikuu cha kuanzisha ugonvi usiokuwa na maana, na kurudisha nyuma hamasa za mpenzi wako kwako.
    Weka akilini sio kila mwanamke sio mwaminifu, jiamini na jiamini unapendwa.

    3. Hauchukui wajibu kwenye makosa yako...
    Wanaume wengi hupenda kurumbana, na wanahisi kurumbana na kutoa shutuma ndio kuwarekebisha wapenzi wao, na ndo jia pekee ya kufanya wapenzi wao wawaheshimu, na saa nyingine haya maono yanawapeleka mbali kiasi kwamba hata wenyewe wakifanya makosa hawajui kuchukuwa wajibu, jambo lolote likitokea ambalo wamesababisha wao hawawezi kukubali kosa, kiasi wanawaona wapenzi wao sio waelewa, maono haya husababisha kuachwa na kukimbiwa na wapenzi,hakuna binadamu atakaye weza kukuvumilia kama hujui kuchukua wajibu na kukubali makosa yako, na inawezekana kabisa baada ya hapo bado wakaendelea kumshitumu msichana kwa kuondoka.
    Ukitaka kukaa na msichana kwenye uhusiano na uendelee kwa muda mrefu jifunze kuchukua wajibu kwenye makosa yako.

    4. Unajishusha kwa kila jambo...
    Unajaribu kumvuta mpenzi wako kwa kujishusha, haulalamiki, haubishani, unabembeleza kila kitu kupita kiasi, saa nyingine kosa umefanyiwa wewe bado tena wewe mwenyewe ndo unaenda kuomba msamaha, hata huwezi kumkaripia na akikuacha na kuhisi wewe uko kama bwege na kwenda kwa mwanaume mwingine bado unalalamika, na ukipata uhusiano mwingine mpya unaendelea kujishusha zaidi.
    Wanawake wanapenda watu wenye msimamo na wanaojiamini, mtu anayeweza kuongoza familia, kama akikuacha akaondoka naomba usimshutumu maana nae anatafuta mwanaume aliye bora ambae hata kama akianzisha familia nae anaweza kuiongoza familia.

    5Haubagui...
    Ukijikuta unaachwa mfululizo, ni kwa sababu haubagui, unahisi labda ukijishusha na kuwa na mpenzi yeyote yule hata kama hamuendani kimawazo na kimaono labda atakaa, hii inakufanya umpate msichana asiye endana nawe na kusababisha mparanganyiko na tofauti za kihisia kati ya wewe na yeye kwenye mahusiano yanayosababisha kuachana kwenu.

    6. Unahisia zako ziko juu mno kupita hali ya kawaida...
    Kuwa na hisia kupitiliza ni moja ya sababu unaendelea kuachwa, unakua unamweka mpenzi wako katika hali tata, maana jambo dogo kutokana na hisia zako zilivyojuu sana unakua unaliona ni kubwa, hii inasababisha ugomvi ambao haupo, na utakua unaona unakosewa katika kila kitu mpenzi wako anachofanya, akili yako inakua inafikiria vitu ambavyo havipo, na kusababisha kutokua na amani kwenye mahusiano, na hii inashusha hamasa kwa mpenzi wako na kujikuta ukiachwa na pia hauta jua hata nini lilikua kosa lako.
    Kama unaendelea kuachwa katika kila mahusiano uliyonayo, ni vizuri ukaanza kuchunguza na kuangalia nini unakosea na kurekebisha tabia zinazopunguza hisia na hamasa kwenye mapenzi, ni muda wa kuanza kufanya mabadiliko.

    No comments