Header Ads

siri ya kuzuia mbu wasikuume?

siri ya kuzuia mbu wasikuume?
Mbu
Watafiti wa masuala ya biolojia kutoka Marekani wamebaini kuwa kupunga mkono kwako ama kujaribu kupiga kofi wadudu kunaweza kupunguza uwezekano wa wadudu hao kukuuma tena.
Watafiti hao kutoka chuo kikuu cha Washington cha Seattle wamebaini kuwa mbu wanaweza kujifunza na kutambua aina fulani ya harufu kupitia mshituko ama kofi.
Matokeo yake wataepuka harufu hiyo wakati mwingine.
"Pale mbu wanapobaini harufu za aina mbali mbali kwa njia ya kujilinda, harufu hizo huwafanya wachukue hatua sawa na wakati wanapopuliziwa dawa ya DEET, moja ya dawa ya kuua mbu," alisema afisa wa ngazi ya juu ya uandishi wa utafiti huo Jeff Riffell, na profesa wa biolojia katika chuo kikuu cha Washington.
"Zaidi ya hayo, mbu hukumbuka harufu waliyozoweshwa kwa siku kadhaa."
Haki miliki ya pichaAFP
Image captionKALI  ZOTE BLOG 
Watafiti tayari walikua wanafahamu kwamba mbu huwa wanachagia ni nani wa kumuuma na nani wasimuume.
Hivyo basi, kuna watu wanaopendelea kuwauma kuliko wengine.
Pia wanafahamika kwa kubadili makao kulingana na msimu, huku wakiwauma ndege msimu wa kiangazi na wanyama na ndege wakati wa majira mengine ya mwaka kwa mfano.
Riffell na wenzake walitaka kubaini zaidi kuhusu namna kujifunza harufu kwa mbu kunachangia katika kuwachagua ni akina nani wanaopendelea kuwauma.
Kama hatua ya kwanza, waliwapatia mafunzo mbu kwa kupanga aina mbili mbili za harufu ya mtu fulani ama mnyama - paka pamoja na kuku kwa mfano - pamoja na mshtuka wa mashine.
Kuhusu mshtuko wa kusababishwa mashine, walitumia mtambo unaosababisha kuwepo kwa upepo mkubwa kwa ajili ya kuchochea mitetemo na msukumo ambao mbu anaweza kuupata wakati mtu anapojaribu kuwapiga.
Mbu
Image captionWatafiti walitaka kubaini zaidi kuhusu namna kujifunza harufu kwa mbu kunavyochangia katika kuwachagua ni akina nani wanaopendelea kuwauma
Haraka wadudu hao wakatambua harufu ya mazingira na msukumo wa mtambo na kutumia taarifa hiyo katika kuamua ni upande gani wa kupepea - ingawa la kushangaza, mbu hawakutambua kuepuka harufu ya jikoni.
Kujifunza miongoni mwa wanyama, kuanzia nyuki hadi binadamu, kunategemea sehemu ya ubongo ya ung'amuzi wa mambo. Uchunguzi wa zaida wa Riffell na kikosi kizima cha watafiti unaonyesha kuwa sehemu hii ya ubongo inayofahamika kama dopamine kwa lugha ya kitaalam ni muhimu katika utambuzi wa mbu.
Kwa ujumla mbu waliobadilishwa maumbile hawana sehemu hii ya ubongo na hivyo kukosa uwezo wa ung'amuzi.
Matokeo haya yanaweza kuwa na athari muhimu katika udhibiti wa mbu na kuenea kwa magonjwa yanayosababishwa na mbu, kulingana na watafiti.

1 comment: