Header Ads

Kuondoka kwa Zuma, kutaleta mabadiliko Afrika Kusini?


Maelfu ya raia wa Afrika Kusini wamekuwa wakiandamana kwa lengo moja: kumuondoa madarakani Rais Jacob Zuma. Lakini kuondolewa kwa Zuma kweli kunaweza kutatua matataizo yote ya nchini humo
Maelfu ya raia wa Afrika Kusini wakiwa wanaandamani kumshinikiza Rais Jacob Zuma kuachia madaraka, inaleta picha kama vile Zuma ndiyo kikwazo pekee kinacholizuia taifa hilo kusonga mbele.
"Zuma lazima aanguke" umekuwa wito maarufu tokea kulipoanza maandamano dhidi ya rushwa na ukosefu wa ajira mwaka 2015. Hata wanachama wengi wa chama chake cha African National Congress (ANC) wamembandilikia Zuma.

Kumuondoa Zuma hata hivyo, huenda lisiwe suluhisho la matatizo yote yanayolikabili taifa hilo kwa mujibu wa wachambuzi.
Chama cha ANC kimejaa wanasiasa wenye mitazamo sawa na Zuma, na matatizo ya kiuchumi ya Afrika Kusini yameingiliana sana na ukosefu wa usawa uliorithiwa tokea wakati wa ubaguzi wa rangi, kiasi ya kwamba hata Zuma akiondolewa madarakani, huenda hatua hiyo isilete mabadiliko makubwa nchini humo.
Sifa ya Zuma imechafuka kutokana na msururu wa kashfa za rushwa, ikiwa ni pamoja na ile inayohusu utumiaji wa fedha za kodi ya umma kuifanyika marekebisho nyumba yake binafsi, na mafungamano ya karibu na familia ya kibiashara na yenye ushawishi mkubwa.

Wakati huo huo mamilioni ya Waafrika Kusini wanaishi makaazi yasiyo halali, na bila ya huduma za msingi, huku ukuaji wa uchumi ukiwa unazorota hadi kufikia asilimia 0.3 mwaka jana na zaidi ya robo ya idadi yote ya watu nchini humo imekosa ajira.

No comments