Header Ads

Marekani inaitaka Korea Kaskazini kuangamiza silaha za kivita

North Korea's leader Kim Jong Un is seen with an intercontinental ballistic rocket in this undated photo released by North Korea's Korean Central News Agency (KCNA) in Pyongyang 30 November 2017.



Marekani ina matumaini ya kuanza kuona shughuli ya kuangamizwa silaha nchini Korea Kaskazini ifikapo mwaka 2020, mwa mujibu wa waziri wa mashauri ya nchi za kigeni Mike Pompeo.
Matamshi yake aliyoyatoa alipofanya ziara nchini Korea Kusini, yanafuataia mkutano kati ya Rais Donald Trump na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un.
Walisaini makubaliano ya kufanya kazi katika kuangamiza kabisa silaha za nyuklia katika rasi ya Korea.
Lakini nakala hiyo imekosolewa kwa kukosa taarifa za kina kuhusu ni lini na ni vipi Korea Kaskazini itaachana na silaha zake.


US Secretary of State Mike Pompeo, right, arrives in Seoul, 13 June 2018Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMike Pompeo (kulia) akiwa Seol

Bw Pompeo alisafiri kutoka Singapore kwenda Seoul ambapo alikuwa akihifahamisha serikali ya Korea Kusini kuhusu matokeo ya mkutano huo.
Alsema bado kuna kazi nyingi ya kufanywa na Korea Kaskazini, "ya kuangamiza silaha ... Tuna matumaini kuwa tutaweza kutimiza hilo ndani ya miaka miwili unusu."
Alisema ana uhakika kuwa Pyongyag ilikuwa inafahamu kuwa shughuli yoyote ya kuangamiza programu yake za nyuklia itahitaji hakikisho.


US President Donald Trump disembarks from Air Force One upon arrival at Joint Base Andrews in Maryland on 13 June 2018Haki miliki ya pichaAFP
Image captionTrumop akiwasili nyumbani baada ya mkutano na Kim

Rais Trump mapema alitangaza kuwa Korea Kaskazini sio tena tisho la nyuklia akisisitiza kuwa kila mtu sasa anaweza kuhisi salama.

Kipi kiliafikiwa kwenye mkutano huo?

Viongozi hao walisema watashirikana katika kujenga uhusiano mpya huku Marekani ikiihakikishia usalama Korea Kaskazini.
Pyongyan nayo itajitolea katika kuangamzia silaha za nyuklia kwenye rasi ya Korea.
Kisha kwenye mkutano na waandishi wa habari Trump akasema kuwa ataiondolewa Korea Kaskazini vikwazo wakati suala la silaha za nyuklia litatatuliwa.


South Korean and US tanks fire live rounds during a joint live-fire military exercise near the demilitarized zone, separating the two Koreas in Pocheon, South Korea. April 21, 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMarekani hufanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi na Korea Kusini na pia Japan

Alisema anaamini kuwa Bw Kim atatekeleza yale ambayo ameyasema.
Alitangaza kusitishwa mazoezi ya kijeshi ambayo hufanyika mara kwa mara kati ya wanajeshi wa Marekani na Korea Kusini katika rasi wa Korea
Hatua hiyo imekuwa ikiitishwa kwa muda na Pyongyang na ilitangazwa bila matarajio kutoka kwa washirika wa Marekani na iliwapata kwa mshangao.
Makao rasmi ya rais wa Korea Kusini ya Blue House baadaye yalisema yalitaka kufahamu maana kamili ya matamshi ya Trump kuhusu kusitisha mazoezi ya kijeshia ya pamoja.

MUSSA NTIMIZI  KUJENGA TABORA MPYA 2018

No comments