Header Ads

Donald Trump amefichua taarifa za siri

Image result for picha ya trump

Gazeti la Washington Post limeripoti kwamba rais Donald Trump amefichua taarifa za siri kuhusiana na wanamgambo wa Dola la Kiislamu kwa maafisa wa Urusi wakati wa mkutano wao wiki 

iliyopita, na kusababisha shutuma kali kutoka kwa Wademocrats na Warepublican. Mshauri wa usalama wa taifa McMaster alizungumza na waandishi habari kukana taarifa hizo.

"Hakuna kitu ambacho rais anakichukulia kwa dhati kabisa kama usalama wa watu wa Marekani. Taarifa hiyo imekuja usiku, kama ilivyoripotiwa, ni uongo. Rais na waziri wa mambo ya kigeni

 wameangalia vitisho kadhaa kwa nchi zetu mbili ikiwa ni pamoja na kitisho kwa usafiri wa anga. Hakuna wakati vyanzo vya 

upelelezi ama mbinu vilijadiliwa."Gazeti hilo la Washington Post limesema mshirika wa upelelezi hakutoa ruhusa kwa Marekani kutoa taarifa hizo kwa maafisa wa Urusi. Shirika la ujasusi la Marekani CIA na ofisi ya mkurugenzi wa idara ya upelelezi ya taifa walikataa kusema lolote jana.


chanzo dw

No comments