Header Ads

Mtandao wa kijamii wa Facebook bado unatumika nchini Thailand, licha ya muda wa mwisho kukamilika


Wathailand ni kati ya watumiaji wakubwa zaidi wa Facebook barani Asia,
Haki miliki ya picha AFP
Image caption Utawala unafuatilia habari kuhusu mfalme mpya Vajiralongkorn
Mtandao wa kijamii wa Facebook bado unatumika nchini Thailand, licha ya muda wa mwisho kukamilika wa kuitaka Facebook, kuondoa taarifa ambazo utawala wa nchi hiyo umezitaka kuwa potovu kwake.
Facebook ilikuwa imepewa muda wa hadi 10:00 (04:00 GMT) kuondoa kurasa 131 ambazo Thailand ilisema zinakiuka sheria zake kali za lese-majeste 

Zaidi ya watu 100 wamefunguliwa mashtaka chini ya sheria hiyo tangu yafanyike mapinduzi ya kijeshi miaka mitatu iliyopita.
Utawala ulitishia kuchukua hatua za kisheria na kuufunga kabisa mtandao wa Facebook.

Baada ya muda uliotangazwa kupita katibu katika kampuni inayosimamia mawasiliano nchini Thailanda, aliwaambia waandishi wa habari kuwa amri za mahakama zimetolewa kwa kurasa 34, na utawala huo ulikuwa ukitafuta amri zingine kwa kusara zingine 97.
Haki miliki ya picha AFP
Image caption Wathailand ni kati ya watumiaji wakubwa zaidi wa Facebook barani Asia
Wathailand ni kati ya watumiaji wakubwa zaidi wa Facebook barani Asia, huku maelfu ya biashara ndogo zikiutegemea mtandao huo kama chomo kikuu cha mauzo.
Ikiwa serikali itatekeleza vitisho vyake na kuwalazimisha watoa huduma za mitandao kuifunga, kutakuwa na malalamiko makubwa nchini humo.

Hata hivyo serikali ina matumaini ya kuhakikisha kuwa hakuna taarifa zinazotajwa kuwa mbaya, zitaruhusiwa kuonekana nchini Thailand licha ya kuwepo changamoto z

No comments