Header Ads

Trump amfuta kazi James Comey



Ikulu ya Marekani ya White House imetangaza jana kwamba rais Donald Trump amemfuta kazi mkurugenzi wa shirika la uchunguzi wa makosa ya jinai FBI James Comey kuhusiana na jinsi 

anavyoshughulikia uchunguzi kuhusiana na barua pepe za Hillary Clinton. Barua kutoka Ikulu ya White House imemfahamisha Comey kwamba kufukuzwa kwake kazi kunaanza mara moja. 

Comey amekuwa akiongoza uchunguzi kuhusu mawasiliano kati ya wasaidizi wa kampeni ya Trump na maafisa wa Urusi kabla ya uchaguzi wa rais mwaka 2016. Mkurugenzi huyo wa FBI 

alikosolewa vikali pale alipotangaza kwamba shirika lake linafungua upya uchunguzi kuhusiana na jinsi Clinton alivyozihifadhi taarifa nyeti kiasi siku chache kabla ya uchaguzi. Trump alisema katika barua yake kwamba Ikulu ya White House tayari inatafuta mtu wa kuchukua nafasi yake.


chanzo dw

No comments