Header Ads

Manchester United kumkosa Rooney



Manchester United hawatakuwa na mshambuliaji namba moja dhidi ya Chelsea
Image captionManchester United hawatakuwa na mshambuliaji namba moja dhidi ya Chelsea
Nahodha wa Manchester United Wayne Rooney ameondolewa katika kikosi kitakachomenyana na Chelsea katika hatua ya robo fainali kombe la FA itakayopigwa leo hii.
Rooney aligongana na mlinzi Phil Jones wakati wa mazoezi na kupata majeraha katika mguu wake, huku Zlatan Ibrahimovic akianza kutumikia adhabu yake ya kukosa michezo mitatu baada ya kumpiga kiwiko mlinzi wa Bournemouth Tyrone Mings.
Washambuliaji Anthony Martial na Marcus Rashford nao pia watakosa mchezo huo kwa kuwa ni wagonjwa.
Zlatan Ibrahimovic (kulia) nae pia atakosa mchezo huo
Image captionZlatan Ibrahimovic (kulia) nae pia atakosa mchezo huo
Meneja wa Chelsea Antonio Conte anasema wachezaji wa kikosi chake wote ni wazima.
Manchester united hawatakuwa na mshambuliaji wa kikosi cha kwanza leo

No comments