Header Ads

Ukosefu wa dhana bora za kilimo na ukosefu wa elimu juu ya kuongeza thamani ya mazao


Image result for vifaa vya kilimo

Ukosefu wa dhana bora za kilimo  na ukosefu wa elimu juu ya kuongeza thamani ya mazao umetajwa kuchangia kwa kiasi kikubwa wanannchi wa pembezoni kushindwa kulima kilimo cha kisasa hali inayochangia  kuwepo kwa   uhaba wa chakula kila mara 
Hayo yamebainishwa hivi karibuni na wakulima kutoka kata ya Mwadui Lohumbo kwenye kikao kilichofanyika wilayani kishapu chini ya  mtandao wa jinsia tgnp wakati kikundi cha taarifa na maarifa kikiwasilisha changamoto mbali mbali zinazowakabili katika kata yao
Taarifa ya kituo hicho iliyowasilishwa na bi LUCIA DAUD imesema kuwa  changamoto ya dhana bora za kilimo ,soko pamoja na wanaume kutojihusisha na kilimo  huchangia kukosa mazao ya kutosha kwa ajili ya chakula na biashara  na kuiomba serikali kuwapatia elimu juu ya kilimo cha kisasa  na kuwatafutia masoko 
                     
Godwin  everygis ni kaimu afisa kilimo wa wilya ya shinyanga amekiri kuwepo kwa tatizo la ukosefu wa elimu kwa wakulima kutokana na idadi ya wataalamu kuwa ndogo katika halmashauri hiyo huku akibainisha hatua wanazochukua kuwasaidia wakulima hao
                                
kikao hicho kilichoandaliwa na tgnp mtandao kimewashirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na wakuu wa idara za halmashauri hiyo
                                                          





No comments