Header Ads

: Klabu gani ina wakati mgumu zaidi msimu wa Krismasi

EPL: Klabu gani ina wakati mgumu zaidi msimu wa Krismasi?

Lakini mechi 11 zinazofuata zitachezwa katika siku 47 pekee.
Kila moja kati ya klabu zilizo kwenye Ligi Kuu itacheza mechi nne wakati wa sikukuu - mechi moja zaidi ya msimu uliopita.
Msimu uliopita, kila klabu ilikuwa na wiki ya kupumzika kabla ya mechi za Boxing Day isipokuwa Everton.
Mwaka huu, Leicester City watacheza mechi nne - kati ya 23 Desemba na 1 Januari - kipindi cha saa 213.
West Ham, nao watacheza mechi zao nne kwa mwendo wa aste aste kiasi, saa 294 na dakika 45.
Arsene WengerHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMsimu huu klabu ya Arsene Wenger ina nafuu zaidi ya klabu nyingine
Hii ni baada ya mechi yao ya Mkesha wa mwaka Mpya dhidi ya Tottenham kuhamishwa hadi 4 Januari kwa sababu za kiusalama.
Hilo limewapa karibu siku tatu za ziada za kupumzika.
Je, mpangilio kwa klabu mbalimbali ukoje?

No comments