Header Ads

Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara klabu ya Yanga

Image result for PICHA YA YANGA

Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara klabu ya Yanga, kupitia kwa msemaji wake Dismas Ten imekiri kuwa kupata matokeo dhidi ya Mbao FC imekuwa ni jambo mgumu lakini wamejipanga vyema kwa mchezo wa Jumapili.
Ten amekiri ugumu huo wakati akiongelea maandalizi ya Yanga kuelekea mchezo huo ambao utapigwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
“Hatujawahi kupata matokeo dhidi ya Mbao FC, imekuwa ni mechi ngumu kila tunapokutana nao lakini tumejipanga kuhakikisha tunapata hizo alama tatu kabla ya kwenda kwenye Kombe la Mapinduzi”, amesema Ten.
Yanga imekuwa ikipata wakati mgumu inapokutana na Mbao FC tangu ilipopanda daraja misimu miwili iliyopita ambapo katika mechi nne za ligi Yanga haijashinda hata mechi moja.
Yanga kwasasa inashika nafasi ya tatu ikiwa na alama 22 nyuma ya Simba SC na Azam FC zenye alama 23 kila mmoja. Ligi kuu itaendelea wikiendi hii kwa mechi za raundi ya 12 kupigwa. 

No comments