MMESSI AZIDI KUWA JEURI

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola amesema Lionel Messi ndio mtu anayeifanya Barcelona iwe timu yenye nafasi kubwa ya kutwaa Ligi ya mabingwa Ulaya msimu huu.

Guardiola ameyasema hayo alipokuwa akijibu swali kutoka kwa mwandishi wa habari ambaye alimuuliza kuhusu timu yake ya Man City kama ina nafasi kubwa ya kushinda ubingwa wa Ulaya msimu huu.
Pep alimjibu mwandishi kwa kumuuliza swali kuwa, “Ni timu gani anachezea Lionel Messi”, ? Baada ya mwandishi kujibu kuwa ni Barcelona ndipo Guardiola akamwambia kuwa ndio timu yenye nafasi ya kutwaa UEFA.

“Hakuna asiyejua ubora wa Messi, na kama Barcelona inamtumia kwenye eneo la adui unategemea nini kama sio kukumaliza tu mpinzani”, ameeleza Guardiola.
Post a Comment