Header Ads

Viongozi wa Bundesliga Bayern Munich wana kila sababu ya kufurahishwa

Viongozi wa Bundesliga Bayern Munich wana kila sababu ya kufurahishwa na kazi yao wakati wakiingia katika michuano ya katikati ya wiki, baada ya kuimarisha uongozi wao kileleni Bundesliga
1. Bundesliga 15. Spieltag | Borussia Dortmund - Werder Bremen (Reuters/T. Schmuelgen)
Washika mkia Cologne hawajapata ushindi wowote msimu huu na wanalenga kusahau kile kocha Stefan Ruthenbeck alielezea kuwa ni hali "yenye uchungu” hapo jana, wakati walipofungwa mabao manne kwa matatu na washika mkia wenzao Freiburg, hata wakati walikuwa wanaongoza kwa mabao matatu kwa bila kwenye mchezo huo. Cologne watacheza dhidi ya Bayern Munich siku ya Jumatano. Bayern wanaongoza msimamo wa ligi na pengo la pointi nane kufuatia ushindi wa moja bila dhidi ya Eintracht Frankfurt. "Pongezi kwa timu. Tulifanya kile tulipaswa kukifanya. Timu ilianza kwa kasi sana na tulipambana kwelikweli na kuonesha kandanda zuri. Tulicheza vizuri kwa dakika 90 na hivyo nivdyo tulitaka kufanya. Na kwa Bayern kupata ushindi wa moja bila kupitia nafasi moja tu, hilo linaweza kutokea
Borussia Dortmund - Vorstellung Peter Stöger, neuer Trainer (Getty Images/Bongarts/C. Koepsel)
Stoeger ana kibarua katika BVB
Kocha wa zamani wa Cologne Peter Stoeger alipewa jana majukumu ya kuliokoa jahazi la Borussia Dortmund na kazi yake ya kwanza itakuwa mchuano mkali ugenini dhidi ya Main hapo kesho Jumanne. Dortmund wako katika nafasi ya nane na wameshinda moja tu kati ya mechi 13 zilizopita katika mashindano yote chini ya kocha aliyetimuliwa jana Peter Bosz. Dortmund ilizabwa na Werder Bremen mabao mawili kwa moja katika mechi ya mwisho ya Bosz ambaye alisema vijana wake hawakujiamini "Leo nadhani pia hatukucheza vizuri kiakili, hasa katika kipindi cha kwanza. Hii haimaanishi tu katika mapambano, lakini pia jinsi tulivyoshambulia na tulivyocheza katika ulinzi. Hivyo basi unawapa jukumu wachezaji wengine. Tunapaswa kuwa na wasiwasi kuhusu hilo kwa sababu sio vizuri".

No comments