Header Ads

FIFA yatoa Ratiba ya vilabu


Image copyrightGETTY
Image captionRais wa shirikisho la soka ulimwenguni Gianni Infantino
Shirikisho la soka Ulimwenguni (FIFA) limetoa Ratiba ya Kombe la Dunia kwa Klabu ambalo litadhaminiwa na Alibaba E-Auto na kufanyika huko Japan kati ya Desemba 8 na 18.Mashindano haya yatashindaniwa na Klabu 6 Mabingwa wa Mabara pamoja na Mwakilishi kutoka Nchi Mwenyeji Japan.
Mechi za Mashindano haya zitachezwa huko Suita City Football Stadium Mjini Osaka na International Stadium Yokohama, Mjini Yokohama ambako pia ndipo itachezwa Fainali .
Hadi sasa Klabu 3 zimeshathibitika kucheza michuano hiyo ambazo ni Real Madrid, Mabingwa wa Ulaya, waliotwaa Ubingwa wao Mwezi Mei, na Timu nyingine ni Club America ya Mexico na Auckland City FC ya Mexico Bara la Oceanic ambazo zilitwaa Ubingwa wao Mwezi Aprili.

No comments