Header Ads

Timu ya Mpira wa Miguu Ufukweni ya Tanzania imepangwa kucheza na Ivory Coast kati ya Agosti 26, 27 au 28, 2016


Soka
Image captionWachezaji wakicheza soka ya ufukweni
Timu ya Mpira wa Miguu Ufukweni ya Tanzania imepangwa kucheza na Ivory Coast kati ya Agosti 26, 27 au 28, 2016 kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2017 zitakazofanyika Lagos, Nigeria.
Mchezo wa marudiano unatarajiwa kufanyika kati ya Septemba 16, 17, au 18.
Fainali za Mpira wa Miguu Ufukweni ambazo zitafahamika pia kama 2016 CAF Beach Soccer Championship, zitafanyika kuanzia Desemba 13 hadi 18, 2016 jijini Lagos, Nigeria kwa kushirikisha timu nane.
Image copyrightBBC
Tayari Nigeria imepasishwa kuwa mshiriki kwa sifa ya uenyeji wake. Timu nyingine 14 zinawania kucheza fainali hizo.
Timu nyingine zinazowania ni Cape Verde v Senegal, Uganda v Misri, Liberia v Morocco, Kenya v Ghana, Msumbiji v Madagascar, Sudan v Libya.

No comments