Jeshi la polisi Kanda maalumu ya Dar es salaam limeanza uchunguzi wa tukio la kupigwa kwa mwandishi wa habari wa kituo cha Wapo Radio, Silas Mbise ambapo pia limemtaka mwandishi huyo aende kutoa taarifa katika kituo cha polisi ili uchunguzi uweze kufanyika.
Taarifa hiyo imetolewa leo na Kamanda Maalumu wa Kanda ya Dar es salaam, Lazaro Mambosasa.