Header Ads

Rais dkt john pombe magufuli amesema amebaini uingizwaji wa makontena ishirini kila siku ya sukari



Image result for RAISI MAGUFULI

Rais dkt john pombe magufuli amesema amebaini uingizwaji wa makontena ishirini kila siku ya sukari ya magendo katika mpaka wa sirali mkoani mara.
Akizungumza na vyombo vya habari ikulu  jijini dar es salaam mara baada ya kutoka katika mazungumzo ya faragha na mgeni wake rais wa Uganda yoweri mseven  amesema kuwa tayari ameshawaagiza mawaziri husika kwenda kufuatilia tatizo na kuchukua hatua zinazostahili.

Rais dkt john pombe magufuli amesisitiza pia kuwa mahusiano ya Tanzania na Uganda yapo imara na miradi ya maendeleo inayotekelezwa na nchi hizo ukiwemo mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta gaph kutoka hoima nchini Uganda hadi tanga Tanzania unaendelea vizuri.

Kwa upande wake raisi yoweri mseveni wa Uganda amesema pamoja na mambo mengine amekuja kumpa taaarifa ya mkutano wa BRICS uliofanyika nchini afrika ya kusini.


Raisi Magufuli amekutana na rais mseveni wa Uganda ambaye ametembelea Tanzania kwa ziara ya kikazi ya siku moja


No comments