Header Ads

Watu zaidi ya 100 wafariki baada ya ndege kuanguka Havana

Wreckage of the Boeing 737 that crashed shortly after take off from Jose Marti International Airport in Havana, Cuba, 19 May 2018


Watu zaidi ya 100 wamefariki dunia baada ya ndege ya kuwabeba abiria aina ya Boeing 737 kuanguka na kulipuka karibu na uwanja mkuu wa ndege wa Cuba mjini Havana, katika mkasa mbaya zaidi wa ndege nchini humo katika miongo kadha.
Wanawake watatu waliondolewa kutoka kwenye mabaki ya ndege hiyo wakiwa hai, lakini taarifa zinasema wamo hali mahututi.
Ndege hiyo, ambaye iliundwa karibu miaka 40 iliyopita, ilikuwa imewabeba abiria 104 na wahudumu sita wa ndege.
Ndege ndefu zaidi duniani yapata ajali
Serikali ya Cuba imeanzisha uchunguzi, na kutangaza siku mbili za maombolezo ya kitaifa.
Ndege hiyo Boeing 737-201 ilianguka saa sita na dakika nane mchana Ijumaa, muda mfupi baada ya kupaa kutoka Havana.
Ndege hiyo ilikuwa kwenye safari ya ndani ya nchi kutoka Havana kwenda Holguin, mashariki mwa Cuba.
Wahudumu wote sita wa ndege hiyo walikuwa raia wa Mexico lakini wengi wa abiria ni raia wa Cuba.
Taarifa zinasema kulikuwa na abiria watano raia wa kigeni.
"Kumekuwa na ajali ya ndege ya kusikitisha sana. Taarifa tulizo nazo ni za kutamausha, yamkini kuna idadi kubwa sana ya waathiriwa," Rais wa Cuba Miguel Diaz-Canel alisema baada ya kutembelea eneo la ajali.

kamanda wa jeshi la posi tabora wilbrod mutafungwa

No comments