Header Ads

Asilimia 87 ya Watanzania wapo tayari kulipa ada ili kupata elimu bora

Taasisi ya Twaweza leo May 17, 2018 imetoa utafiti wake kuhusu masuala ya elimu ambapo imebainika kuwa mitazamo ya wananchi kuhusu elimu bure imebadilika kwa kiasi kikubwa ndani ya miaka 12 iliyopita.
Meneja Utetezi wa Twaweza, Anastazia Lugaba amesema kuwa asilimia 87 ya watanzania kupitia utafiti huo kwa mwaka 2017 uliopewa jina ‘Elimu bora au Bora Elimu? waitakayo watanzania’ wapo tayari kulipia ili kupata ubora kwenye elimu tofauti na mwaka 2005 ambapo (56%) ya wananchi walisema kuwa ni bora elimu itolewe bure kwa watoto hata kama kiwango cha elimu ni cha chini.
“Tunaelewa kwamba tumeelekeza watoto wapate elimu bure, japo tumeondoa michango na pia tumeondoa ada lakini changamoto kwenye sekta ya elimu zinaonekana kuwa ni nyingi na kubwa sana, kwasababu walimu ni wachache na wanafunzi ni wengi sana” amesema Lugaba
Taarifa ya Twaweza inaeleza kuwa matokeo hayo yanatokana na takwimu zilizokusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,789 kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania bara pekee
.
askofu wa jimbo la tabora kwa makanisa ya E.A.G.T MAHUNA CHARSE achangua viongozi


No comments