Header Ads

Watu 9 pekee anao wakubali Rais Magufuli



Imekuwa ni kawaida kwa watu kufollow watu wengine kwenye mitandao ya kijamii, na mara nyingi huwa kwa sababu mbali mbali, na kujikuta kuwa na maelfu ya watu wanaowafollow.
Lakini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, kwenye acount yake ya twitter ambayo mara nyingi huitumia, amefollow watu 9 tu dunia nzima, huku watanzania wawili tu wakipata bahati ya kuwa 'followed' na Rais Magufuli.
Watu hao ni 
1. Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia kwa Afrika, Makhtar Diop
2.  Waziri Mkuu wa India Narendra Modi . 
3. Rais wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni.
4. Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari. 
5. Rais wa Rwanda, Paul Kagame 
6. Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta 
7. Umoja wa Mataifa 
8. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira, Januari Makamba.
9. Rais Mstaafu wa awamu ya nne wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.


Watu hao aliowafollow Rais Magufuli nao wamefollow watu zaidi ya 10, na wengine kufikisha hata watu elfu na zaidi ya wanaowafollow.


No comments