Header Ads

Ennahda yatangaza kushinda uchaguzi Tunisia

Kommunalwahlen in Tunesien (picture-alliance/AP Photo/H. Dridi)
Baada ya vituo vya kupigia kura kufungwa majira ya saa 12 jioni kwa saa za Tunisia, afisa wa ngazi ya juu wa chama cha Ennahda, Lofti Zitoun alisema kuwa chama chake kimeshinda kwa asilimia tano zaidi kikiwa mbele ya chama  cha upinzani cha Nidaa Tounes.
Vyama vya Ennahda na Nidaa Tounes ni vyama washirika katika serikali ya muungano wa kitaifa na vilikuwa vinatarajiwa kutawala katika uchaguzi huo uliocheleweshwa kwa muda mrefu, ambao utashuhudia maafisa 350 wa manispaa kwa mara ya kwanza tangu baada ya vuguvugu la maandamano ya kupigania demokrasia kwenye nchi za Kiarabu mwaka 2011, yaliouondoa madarakani utawala wa kimabavu uliodumu kwa miongo kadhaa.
Zawadi kubwa Ennahda
Zitoun amesema matokeo hayo ya uchaguzi ni zawadi kubwa kwa Ennahda chama chenye uvumilivu na kinachozingatia demokrasia na kwamba chama hicho kilikuwa kikitaka kuwepo kwa makubaliano.
Aidha, msemaji wa Ennahda, Imed Khemiri amesema chama hicho kitaendelea kuhakikisha panakuwepo na makubaliano na washirika wao. Kauli hiyo ameitoa mbele ya wafuasi wa Ennahda, waliokuwa wamekusanyika nje ya makao makuu ya chama hicho huku wakiimba nyimbo za mapinduzi za mwaka 2011.
Afisa wa chama cha Nidaa Tounes, Borhan Bsais amesema chama chake kiko nyuma ya Ennahda kwa asilimia tatu hadi tano. Amesema ni muhimu kuwa vyama hivyo viwili vimeshinda na muhimu kwa ajili ya usawa wa kisiasa nchini Tunisia.

No comments