Header Ads

BAYERN MUNICH MDOMONI MWA REAL MADRID LEO

Mshambuliaji Arjen Robben wa Bayern Munich ataukosa mchezo wa timu yake leo ikikipiga dhidi ya Real Madrid katika nusu fainali ya pili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Bayern Munich wanaingia katika mchezo huo wakionekana vibonde dhidi ya Real Madrid ambao wapo mbele kwa mabao 2-1, ushindi walioupata katika mchezo wa awali.
Cristiano Ronaldo wa Real Madrid amefunga mabao 9 dhidi ya Bayern Munich, licha ya kuwa mchezo uliopita hakufunga lakini anatarajiw akuwa hatari katika mchezo wa leo.
Hakuna timu ambazo zimekutana mara nyingi katika Champions League kama Real Madrid na Bayern Munich, hadi hizi sasa zimekutana mara 26, Bayern Munich ikishinda mara 11 huku Real Madrid ikishinda 12.
Uwanja wa Santiago Bernabeu ndiyo mahala pachungu zaidi kwa wapinzani katika Champions League, katika dimba hilo Real Madrid wamefunga katika michezo yao 41 ya mwisho ya CL na mechi pekee waliyoshindwa kufunga ilikuwa dhidi ya Barcelona mwaka 2011.
Mbaya zaidi kwa Bayern Munich ni kwamba wanakwenda ugenini katika kipindi ambacho wamecheza michezo 13 ya Champions League ya ugenini na yote wameruhusu bao, huku mshambuliaji wao tegemezi Robert Lewandowski akiwa hajafunga katika mechi 4 zilizopita za CL.


Mshambuliaji Arjen Robben wa Bayern Munich ataukosa mchezo wa timu yake leo ikikipiga dhidi ya Real Madrid katika nusu fainali ya pili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Bayern Munich wanaingia katika mchezo huo wakionekana vibonde dhidi ya Real Madrid ambao wapo mbele kwa mabao 2-1, ushindi walioupata katika mchezo wa awali.
Cristiano Ronaldo wa Real Madrid amefunga mabao 9 dhidi ya Bayern Munich, licha ya kuwa mchezo uliopita hakufunga lakini anatarajiw akuwa hatari katika mchezo wa leo.
Hakuna timu ambazo zimekutana mara nyingi katika Champions League kama Real Madrid na Bayern Munich, hadi hizi sasa zimekutana mara 26, Bayern Munich ikishinda mara 11 huku Real Madrid ikishinda 12.

Uwanja wa Santiago Bernabeu ndiyo mahala pachungu zaidi kwa wapinzani katika Champions League, katika dimba hilo Real Madrid wamefunga katika michezo yao 41 ya mwisho ya CL na mechi pekee waliyoshindwa kufunga ilikuwa dhidi ya Barcelona mwaka 2011.
Mbaya zaidi kwa Bayern Munich ni kwamba wanakwenda ugenini katika kipindi ambacho wamecheza michezo 13 ya Champions League ya ugenini na yote wameruhusu bao, huku mshambuliaji wao tegemezi Robert Lewandowski akiwa hajafunga katika mechi 4 zilizopita za CL.




No comments