Header Ads

Dawa ya kutibu upara yapatikana


Mtu mwenye upara

Dawa ya kutibu upara imegunduliwa kwa kutumia dawa ya kutibu mifupa iliodhoofika
Watafiti waligundua kwamba dawa hiyo ina athari kubwa katika mashina ya nywele katika maabara kwa kuzipatia nguvu nywele kumea. Dawa hiyo inashirikisha vipengele vinavyolenga protini ambayo hutumika kukatiza umeaji wa nywele na hivyobasi kusababisha upara.
Kiongozi wa mradi huo Dkt. Nathan Hawkshaw kutoka chuo kikuu cha Manchester alisema inaweza kuleta tofauti kwa watu wanaokabiliwa na ukosefu wa nywele
Ni dawa mbili pekee ambazo hutumika kutibu upara
  • minoxidil, kwa wanaume na wanawake
  • finasteride, kwa wanaume pekee
Dawa zote mbili zina madhara na hukosa kufanya kazi mara nyengine hivyobasi waathiriwa hupendelea kufanya upandikizaji wa nywele badala yake
Utafii huo uliochapishwa katika jarida la PLOS Biology ulifanywa katika maabara, huku sampuli zikiwa na nywele kutoka kwa zaidi ya wagonjwa 40 wa kiume wanaotaka kupandikizwa nywele
Na Dkt. Hawkshaw aliambia BBC kwamba jaribio litafanywa kuona iwapo tiba hiyo inafanya kazi na ni salama kwa watu

Presentational grey line

Ni nini kinachosababisha kupotea kwa nywele?
Kupotea kwa nywele ni swala la kila siku na sio tatizo la kukutia wasiwasi. Baadhi ya nywele ni za kudumu huku nyengine zikiwa za muda mfupi.

Presentational grey line

Msemaji wa muungano wa madaktari wa ngozi nchini Uingereza aliambia BBC: Huu ni utafiti muhimu sana
"Watafiti wanasema kuwa kupotea kwa nywele ni tatizo la kawaida na linaweza kuathiri afya yako ikiwemo kukosa kujiheshimu na kujiamini.
''Utafiti zaidi utahitajika kufanywa kabla ya kutumika na watu walio na tatizo la kupoteza nywele''.
Kwa watu wenye tatizo la kupotea kwa nywele, tiba imepatikana.
Hatua hiyo inawapatia waathiriwa afueni kwa kuwa kuna chaguo la dawa ambazo zinaweza kutibu.

No comments