Header Ads

shambuliaji wa Uingereza na Leicester Jamie Vardy amekubali kuweka kandarasi mpya na viongozi wa ligi ya Uingereza Leicester.

Vardy akubali kandarasi mpya na Leicester

Image copyrightREUTERS
Image captionJamie Vardy
Mshambuliaji wa Uingereza na Leicester Jamie Vardy amekubali kuweka kandarasi mpya na viongozi wa ligi ya Uingereza Leicester.
Leicester imesema kuwa mchezaji huyo wa miaka 29 ambaye mabao yake yameisaidia klabu hiyo kushinda taji la ligi ya Uingereza msimu uliopita ameongeza kandarasi yake hadi miake minne na klabu hiyo.
''Pande zote mbili zinatumai tangazo hilo litamaliza uvumi wa hivi karibuni kuhusu hatma ya Jamie'',taarifa ya klabu imesema.
Vardy alitarajiwa kununuliwa na klabu ya Arsenal kwa kitita cha pauni milioni 20 na Arsenal kabla ya kuanza kwa michuano ya Euro 2016 huku The Gunner ikitoa kitita cha pauni 120,000 kila wiki kwa mchezaji huyo.
Leicester nayo ilijibu kwa kutaka kumpatia pauni 100,000 kwa wiki.

No comments