Header Ads

Chama cha Mapinduzi CCM kata ya Ndembezi katika Wilaya ya Shinyanga Mjini imefanya usafi wa Mazingira

 Image result for picha ya ccm



Jumuiya ya vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM kata ya Ndembezi katika Wilaya ya Shinyanga Mjini imefanya usafi wa Mazingira katika kituo cha afya cha Ngokolo Mjini Shinyanga,ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka arobaini ya Chama hicho ambapo kilele chake ni Februari 05,mwaka huu.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya vijana wa ccm-uvccm kata ya  Ndembezi DOTTO JOSHUA  amesema maadhimisho ya Chama hicho kwa mwaka huu 2017 yatafanyika kwa utaratibu wa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo usafi,badala ya mikutano,ngoma na Maandamano kama ilivyozoeleka.

Mwenyekiti huyo amesema Miaka arobaini tangu kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM, wananchi wameendelea kuwa na  imani na Chama hicho tawala ambacho kimepiga hatua mbalimbali za mafanikio.


Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM  wilaya ya Shinyanga mjini CHARLES SANGURA amesema kuelekea kilele cha maadhimisho hayo Chama na  Jumuiya zake,ikiwemo wazazi,UWT,na vijana  watafanya shughuli mbali mbali za kijamii ikiwemo utoaji wa Elimu, usafi wa mazingira, na upandaji wa miti.

No comments