Header Ads

Kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone, amesema kwamba hashangai kuona vilabu


Kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone, amesema kwamba hashangai kuona vilabu vyenye uwezo wa kumsaini Antonie Griezman vikimuwinda mchezaji huyo, Simeone amesema hatomzuia mchezaji yoyote atakayetaka kuondoka Vicente Calderon.


Antonie Griezmann amekuwa akihusishwa na kutaka kuhamia Manchester United mwishoni mwa msimu huu, na mwenyewe amekuwa akizungumzia uwezekano wa kucheza pamoja na mchezaji mwenzie wa timu ya taifa ya Ufaransa katika ngazi ya klabu.
Taarifa kutoka Uingereza zinasema kwamba, Manchester United watakuwa tayari kumsajili Griezmann endapo Atletico watakubali kumuuza kwa ada inayotajwa kufikia €100m.

No comments