Header Ads

kuepusha matukio ya kutupwa watoto

Image result for mtoto atupwa chooni
 zimeshauri kutoa adhabu stahiki kwa wanaume wanaobainika kutelekeza watoto  au wanawake wenye ujauzito wao,ili kuepusha  matukio ya utoaji wa mimba,kuuawa,kutupwa na kutelekezwa watoto hasa wachanga.. 

Mkurugenzi wa Shirika la  AGAPE JOHN MYOLA  amesema ili kuepusha matukio ya kutupwa watoto,mamlaka hizo ikiwemo Polisi,Mahakama, na Ustawi wa Jamii zina wajibu wa  kupokea, kusikiliza,na kuwasaidia   wanawake waliotelekezewa mimba au watoto,badala ya kuwapuuza.

Hata hivyo amewaomba wasichana na wanawake kutochukua maamuzi magumu ya kutoa mimba au kuua watoto kwa sababu ya kutelekezwa,na badala yake wanapaswa kuwa wawazi ili waweze kupatiwa ushauri nasaha 

Mkurugenzi huyo wa shirika la AGAPE ameshauri watoto wa kike kutokatishwa tamaa  na badala yake wanapaswa kujitambua,na kufahamu kuwa wana thamani kubwa katika Jamii kwani wanategemewa kulitumikia Taifa.
                                                                       

No comments