Header Ads

Shirika la habari la Liberty limesema litanunua biashara ya mashindano ya magari ya langalanga ya Formula 1,

KALI ZOTE BLOG

Formula 1Image copyrightEPA
Image captionKampuni ya Liberty Media italipa $4.4bn
Shirika la habari la Liberty limesema litanunua biashara ya mashindano ya magari ya langalanga ya Formula 1, katika mkataba wa thamani ya dola bilioni nne unusu za kimarekani.
Liberty, ambayo inamilikiwa na bilionea John Malone, katika hatua za kwanza itanunua hisa chache katika kampuni hiyo kutoka kwa muungano wa wawekezaji wanaouza hisa.
Baadaye, itachukua udhibiti kamili iwapo maafisa wasimamizi wa mashindano wataidhinisha ununuzi.
Liberty imesema Bernie Ecclestone, ambaye amedhibiti mashindano hayo kwa muda mrefu, ataendelea kuwa afisa mkuu mtendaji wa Formula One.
Bernie EcclestoneImage copyrightGETTY IMAGES
Image captionBernie Ecclestone (kulia) akiwa na mkuu wa timu ya Red Bull Christian Horner.
Chase Carey, naibu mwenyekiti wa 21st Century Fox, atakuwa mwenyekiti mpya

No comments