Feyisa Lilesa aliyeonyesha alama ya X
KALI ZOTE BLOG
Mwanariadha wa
Ethiopia na mshindi wa medali ya fedha wa mbio za marathon za Olimpiki
Feyisa Lilesa aliyeonyesha alama ya X alipomaliza mbio zake amewasili
nchini Marekani.
Hii inatokea takriban wiki tatu baada ya taarifa
yake kugonga vichwa vya habari kuhusu alipokunja juu mikono yake kwa
alama ya X juu ya kichwa chake wakati akimaliza mbio hizo mjini Rio.
Alama hiyo ni ishara ya kuipinga serikali inayotumiwa na waandamanaji
katika jimbo anakotoka la Oromia na imeifanya dunia kutambua wimbi la
maandamano ya upinzani nchini Ethiopia.
Bw Feyisa iwapo atarejea
nyumbani atakuwa na hofu ya maisha yake ama anaweza kukabiliwa na
kifungo cha gerezani kutokana na tendo hilo alilolifanya.
Aliishi
nchini Brazil baada ya kushinda medali yake katika siku ya mwisho ya
michezo hiyo tarehe 21 Agosti, ambapo alikataa kurejea nyumbani na timu
ya wanariadha wengine wa Ethiopia.
Serikali ya Ethiopia ilisema itampokea nyumbani kama shujaa.
Bw Feyisa alisema kuwa ameazimia kuomba uhamiaji nchini Marekani.
Kwa sasa yuko mjini Washington DC baada ya kupewa kibali cha dharura cha kuishi nchini humo.
Ukurara
wa mtandao wa kijamii umefunguliwa na waethiopia wanaoishi Marekani kwa
ajili ya kutafuta fedha za udhamini wa mahitaji ya maisha yake .
Ndugu na jamaa zake bado wanaishi nchini Ethiopia.
Post a Comment