KENYA YA RUHUSU WA SICHANA WA KIISLAM KUVAA JUBA
Wasichana wa kiislam wanaosoma shule nchini Kenya wanapaswa
kuruhusiwa kuvaa hijab kama sehemu ya sare zao za shule , imeamuru
mahakama ya rufaa.
Uamuzi huo wa kihistoria uliotolewa na majaji
watatu umekuja baada ya kanisa la kimethodist kupinga muongozo kutoka
kwa mamlaka za nchi hiyo kuwaruhusu wasichana wa shule wa kiislamu kuvaa
hijab ama vilemba katika shule yake.
Wanafunzi wa kiislam katika
shule ya sekondari ya St Paul Kiwanjani School kaunti ya Isiolo
walipigwa marufuku kuvaa hijab na suluari nyeupe pamoja na sare ya
shule.
Kanisa hilo lilidai kuwa uamuzi wa kuwaruhusu wanafunzi
wasichana wa kiislamu kuvaa mavazi tofauti umesababisha uhasama
miongoni mwa wanafunzi.
Mahakama ya juu iliunga mkono kanisa na kusema kuwa wasichana hawawezi kuvaa hijkabu shuleni.
Lakini
majaji katika mahakama ya rufaa wamesema kuwa ni jukumu la wanaotoa
elimu kukubali maadili na kanuni za utu, na za matabaka mbali mbali ya
watu, na bila ubaguzi , limeripoti gazeti la Star nchini Kenya.
Kwa
mujibu wa gazeti la East African Standard, majaji hao waliongeza
kusema kuwa vazi la kidini haliwezi kulinganishwa na mtindo wa vazi
unaokwenda na wakati
Shule za kitaifa huruhusu wasichana kuvaa hijab.
Post a Comment