Header Ads

MWANAMKE MMOJA AKAMATWA AKIFANYA BIASHARA HARAM

JESHI la Polisi katika Mkoa wa Mara linamshikilia Juritha Lucas (60), mkazi wa Kijiji cha Masinki Wilaya ya Serengeti mkoani humo, kwa tuhuma ya kufanya biashara haramu ya kuuza binadamu kinyume cha sheria.






Kamanda wa Polisi mkoani Mara, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Ramadhani Ng'anzi, aliliambia gazeti hili kwa njia ya simu kutoka mjini Musoma jana kuwa, mwanamke huyo alikamatwa na polisi akiwa na mabinti watano wenye umri kati ya miaka 15 na 23 aliokuwa anataka kuwauza.

Kamanda Ng'anzi alisema mabinti hao ni wakazi wa kijiji cha Muruvyagiza, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, ambako ndiko mwanamke huyo aliwatoa na kuwasafirisha hadi katika kijiji cha Masinki wilayani Serengeti, kwa nia ya kuwauza kwa kuwaozesha kwa wanaume kwa bei kati ya Sh 150,000 hadi Sh 300,000 kila mmoja, kulingana na umri, uzuri na tabia ya binti husika.

No comments