Header Ads

SIMBA jana iliendeleza ubabe kwa Mtibwa Sugar baada ya kuifunga mabao 2-0

SIMBA jana iliendeleza ubabe kwa Mtibwa Sugar baada ya kuifunga mabao 2-0 katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.




Mechi hiyo iliyokuwa ikitarajiwa kuwa ya vuta nikuvute, Simba ilionekana kutawala mchezo katika vipindi vyote viwili. Ushindi huo unaifanya Simba kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ikifikisha pointi 10 sawa na Azam katika mechi nne ilizocheza, ikishinda tatu na kutoka sare moja.

Iliichukua Simba dakika 52 kuandika bao la kuongoza katika mechi hiyo likifungwa na Ibrahim Ajib aliyefunga kwa kichwa akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na Mohamed Hussein, ‘Zimbwe Jr’.
Bao hilo lilizidi kuamsha safu ya ushambuliaji ya Simba ambayo ilikuwa ikilishambulia lango la Mtibwa Sugar kama nyuki ambapo dakika ya 66 ilipata bao la pili lililofungwa na Mrundi Laudit Mavugo.

Mavugo alifunga bao hilo kwa kazi nzuri iliyofanywa na Mwinyi Kazimoto aliyeambaa na mpira nje ya 18 kabla ya kuachia shuti maridadi lililomkuta Mavugo ambaye hakufanya ajizi akaujaza mpira wavuni.
Mtibwa katika mechi ya jana itabidi ijilaumu kwani pamoja na kubanwa na safu ya ulinzi ya Simba lakini ilipata nafasi kadhaa ikashindwa kuzitumia hasa ile ya dakika ya 16 pale Haruma Chanongo alipounganisha pasi ya Stahmili Mbonde lakini shuti lake liliokolewa na mabeki wa Simba.
Chanongo alikosa bao lingine katika dakika ya 32 kwa pasi ya Mbonde lakini alip
aisha akiwa peke yake na kipa wa Simba Vincent Angban.

Kikosi cha Simba SC: Vincent Angban, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein ‘Zimbwe Jr’, Novaty Lufunga, Method Mwanjali, Jonas Mkude, Shiza Kichuya/Frederick Blagnon, Muzamil Yassin, Laudit Mavugo, Ibrahim Hajib/Jamal Mnyate, Mwinyi Kazimoto/Said Ndemla.
Mtibwa Sugar: Abdallah Makangana, Ally Shomary, Issa Rashid, Cassian Ponera, Salim Mbonde, Shaaban Nditi, Kevin Friday/Mohammed Juma, Ally Yussuf, Stahmili Mbonde, Ibrahim Juma/Hussein Javu, Haroun Chanong

No comments