WANAKIJIJI CHA NHELEGENI KATA YA KIZUMBIbaada ya mtu asiyelikana anayesadikiwa kuwaingilia kimazingara
Wakazi wa
kijiji cha Nhelegani kata ya kizumbi katika manispaa ya Shinyanga wameingiwa na
hofu baada ya mtu asiyelikana anayesadikiwa kuwaingilia kimazingara katika nyumba zao nyakati za usiku na kuiba mali na kisha kuwaingilia kimwili
baadhi ya wanawake
Wakiongea na
mwandishi wa KALI ZOTE BLOG wanakijiji hao wamesema kuwa mtu huyo huingia katika
nyumba za watu usiku wa manane bila wao
kutambua na kisha kuwaibia hasa simu zao za mkononi na kisha kuwaingilia kimwili wanawake
Moja wa
shuhuda wa tukio hilo kwa masharti ya
kutotajwa jina ameiambia KALI ZOTE BLOG
unakuta umelala na mume wako cha
kushangaza unamkuta mwanaume wako kalala chini au nje halafu huyo mtu
anakufanyia mchezo mchafu cha kushangaza wakati mwingine milango na madirisha tumefunga
lakini ukiamka unakuta ipo wazi hakuna sehemu ilyobomolewa na simu zimeibiwa kama sio ushirikina nini jamani) alisema mama
huyo
Kwa upande
wake kamanda wa jeshi la jadi sungusungu katika kijiji hicho bwana NASORO
MALAJA amesema kwa sasa wanaendelea na ulinzi madhubuti na masako mkali kwa
ajili ya kumbaini mtuhumiwa huyo wa wizi
Aidha mwenyekiti
wa kijiji hicho SENI SHIJA amekiri kupokea taarifa hizo na tayari serikali ya
kijiji imekaa kikao ili kutafuta utatuzi , pia amewaomba wakazi hao kuacha
kuamini katika nguvu za giza bali
usumbufu wa vibaka .
Post a Comment