Header Ads

Waziri wa haki Gabon ajiuzulu kupinga matokeo

KALI ZOTE BLOG


Maandamano GabonImage copyrightAFP/GETTY
Image captionMaandamano yalishuhudiwa baada ya Bw Bongo kutangazwa mshindi
Waziri wa haki nchini Gabon Seraphim Moundounga amejizulu kulalamikia utata ambao umegubika matokeo ya uchaguzi wa urais uliofanyika nchini humo wiki moja iliyopita.
Anadaiwa kumuonya Rais Ali Bongo, ambaye alitangazwa mshindi na tume ya uchaguzi, kwamba angefutilia mbali matokeo ya uchaguzi huo iwapo "hayakulingana na uhalisia."
Bw Mondunga ndiye afisa wa juu serikalini kujiuzulu kufuatia mzozo huo kuhusu matokeo ya uchaguzi.
Mamlaka za Gabon zimesema watu watatu wameuawa na zaidi ya 100 kujeruhiwa kwenye ghasia ambapo pia maelfu wamekamatwa.
Baadhi ya taarifa zinasema huenda idadi ya raia waliokufa ikawa juu. Ufaransa imelalamikia hali nchini Gabon na kusema baadhi ya raia wake nchini humo hawajulikani waliko.
Ali Bongo alitangazwa mshindi wa uchaguzi, lakini upinzani ukiongozwa na Jean Ping ulipinga matokeo.
Bw Bongo alipata 49.8% ya kura naye Bw Ping akiwa na 48.2%, tofauti kati yao ikiwa kura 5,594.
Bw Ping alishinda majimbo sita kati ya tisa na ameomba kurudiwa tena kwa shughuli ya hesabu ya kura.
Katika jimbo la Haut-Ogooue, anamotoka Bw Bongo, waliojitokeza kupiga kura walikuwa 99.93% kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na 95% ya kura zilipigiwa rais huyo
Bw Bongo na Bw PingImage copyrightGETTY IMAGES
Image captionBw Ali Bongo na Bw Jean Ping
Idadi ya wapiga kura waliojitokeza majimbo mengine ni 45% na 71%, kwa mujibu wa wizara ya masuala ya Gabon.
Licha ya Gabon kuwa na utajiri wa mafuta, raia wengi wamesalia masikini
Jean Ping ameomba raia kusalia nyumbani kama mgomo dhidi ya utawal

No comments