Header Ads

Juhudi za uokoaji za kuwanasua watalii 45 ambao wamekwama kwenye magari ya kutumia kamba katika mlima wa Mont Blanc, Ufaransa zimeanza tena.

Juhudi za uokoaji za kuwanasua watalii 45 ambao wamekwama kwenye magari ya kutumia kamba katika mlima wa Mont Blanc, Ufaransa zimeanza tena.


Magari ya kamba






Watalii hao walilala usiku wa Alhamisi kwenye kibaridi kikali wakiwa wamekwama juu ya barafu takriban 3,800m (futi 12,468) juu mlimani.
Walikuwa miongoni mwa watu 110 waliokwama baada ya magari hayo kupatwa na hitilafu Alhamisi alasiri.
Inaaminika magari hayo yalikwama baada ya kamba kushikana kutokana na upepo mkali.
Watu 65 waliokolwa kwa kutuia helikopta baadaye Alhamisi lakini juhudi zikasitishwa giza lilipoingia na kukawa na mawingu hivyo kuifanya vigumu kuona.
"Tulilazimika kusitisha juhudi za uokoaji kwa sababu za kiusalama," alisema Georges Francois Leclerc, mkuu wa idara ya uokoaji ya Haute-Savoie.
"Tunatumai tutawapata wote salama Ijumaa asubuhi," alisema ni kuongeza kwamba ni operesheni ngumu sana.

No comments