Maji ya mto yageuka 'rangi ya damu'
KALI ZOTE BLOG
Wachunguzi wa
masuala ya mazingira nchini Urusi wanajaribu kubaini chanzo cha maji ya
mto ulio karibu na kiwanda cha nikeli cha kampuni ya Norilsk Nickel
yamebadilika rangi na kwua na rangi nyekundu.
Picha za maji ya mto Daldykan ambayo yamebadilika rangi zimesambazwa sana katika vyombo vya habari Urusi.
Gazeti
la serikali la Rossiiskaya Gazeta linasema kuvuja kwa bomba la
kusafirisha taka za mchanganyiko wa shaba nyekundu na nikeli huenda
likawa kiini cha maji hayo kubadilika rangi.
Norilsk Nickel ndiyo mzalishaji mkubwa zaidi wa nikeli na palladium duniani.
Kampuni hiyo ina
kiwanda kwa jina Nadezhda karibu na mto Daldykan lakini maafisa wake
wanasema hawajapata dalili zozote za uchafuzi kutoka kwa kiwanda hicho.
Rais wa kampuni hiyo ni bilionea Vladimir Potanin.
Post a Comment