Header Ads

Nyota mpya mlemavu wa Afrika Kusini aibuka




Nyota mpya mlemavu wa Afrika Kusini aibuka



Mahlangu Ntando alimaliza wa pili mbio za 200m





Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Mahlangu Ntando, 14, ameibuka kuwa nyota mpya kutoka kwa michezo ya Olimpiki ya walemavu inayoendelea mjini Rio, Brazil.
Kijana huyo alishinda nishani ya fedha katika mbio za mita 200 kwa walemavu waliokatwa miguu yao juu ya magoti.
Kwa mujibu wa tovuti ya jarida la Runners World, kijana huyo alijua kutembea miaka minne iliyopita.
Ntando alimaliza na muda wa sekunde 23.77 nyuma ya Mwingereza Richard Whithead (23.39).
Afrika Kusini awali ilijivunia nyota mlemavu Oscar Pistorius ambaye alifungwa jela miaka sita baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp kwa kumpiga risasi mara nne Februari 2013.
Ntando amefurahia ufanisi wake: "Sikutarajia ningeshinda nishani lakini nilijua kwamba nikifanya vyema kabisa ningekuwa katika nafasi nzuri."
"Najihisi vyema sana na ningependa kuwashukuru raia wa Afrika Kusini kwa kunipa fursa hii. Shukrani sana kwa wote walionisaidia kufika hapa."
i

No comments