Header Ads

Mahakama Kuu nchini Kenya imebatilisha uamuzi wa serikali ya Kenya

Wakimbizi katika kambi ya Dadaab

Mahakama Kuu nchini Kenya imebatilisha uamuzi wa serikali ya Kenya wa kufunga kambi kubwa ya wakimbizi ya Daadab inayopatikana kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Mahakama imesema waziri wa usalama wa ndani Meja Jenerali mstaafu Joseph Nkaissery alikiuka katiba wakati wa kutoa agizo la kufungwa kwa kambi hiyo.
Jaji JM Mativo amesema agizo la serikali lilibagua na lilikuwa sawa na kuadhibu watu kwa pamoja.
Jaji huyo alikuwa anatoa uamuzi katika kesi iliyowasilishwa na mashirika mawili ya kutetea haki za kibinadamu: Shirika la Taifa la Haki za Kibinadamu na Kituo Cha Sheria, yakisaidiwa na shirika la kimataifa la Amnesty International.
Serikali awali ilitangaza kwamba ingefunga kambi hiyo, ambayo ndiyo kubwa zaidi duniani, tarehe 30 Novemba mwaka 2016. Ilisema hatua hiyo ilifaa ili kulinda Kenya dhidi ya mashambulio ya kigaidi.

No comments