Header Ads

Viongozi wa Dini Mkoani Shinyanga, wamepongezwa



Image result for Mkoani Shinyanga



Viongozi wa Dini Mkoani Shinyanga, wamepongezwa kwa kushirikiana na serikali katika shughuli mbalimbali za kitaifa, kwani wamekuwa  kiungo muhimu na  mchango  mkubwa katika Maendeleo na ujenzi wa  Taifa la Tanzania.
Naibu msajili wa Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga SEKELA MWAISEJE ameyasema hayo Jana kwenye kilele cha wiki ya sheria nchini,kwamba viongozi wa dini wamekuwa na ushirikiano wa dhati katika shughuli mbali mbali za kitaifa
MWAISEJE amesema mchango wa viongozi wa dini katika  maendeleo ya Taifa  unapaswa kuthaminiwa na kuheshimiwa.
Katika maadhimisho ya wiki ya Sheria nchini katika viwanja vya Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga,viongozi wa dini kutoka madhehebu mbali mbali walihudhuria ambapo Kabla ya kuanza kwa shughuli hiyo,viongozi hao  walitoa sala na dua kwa lengo la kuiombea idara ya mahakama,wadau wa sheria,nchi, na viongozi wa serikali.
                                  

Katika taarifa yake Jaji mfawidhi mahakama kuu kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga mheshimiwa RICHARD KIBELA amewataka mahakimu kutumia adhabu mbadala katika baadhi ya kesi ili watuhumiwa waweze kuwa nje wakiendelea na shughuli za kukuza uchumi,badala ya hukumu ya kifungo gerezani.

No comments