Header Ads

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Buluba iliyopo mjini Shinyanga wamesema mimba mashuleni husababisha madhara mbalimbali ikiwa ni Pamoja na kuwepo kwa ongezeko la watoto wa mitaani.

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Buluba iliyopo mjini Shinyanga wamesema mimba mashuleni husababisha  madhara mbalimbali ikiwa  ni Pamoja na kuwepo kwa ongezeko la watoto wa mitaani.





Image result for SHINYANGA
Add caption




Wakizungumza na KALI ZOTE BLOG leo,wamesema mimba mashuleni husababisha kukatisha malengo,ongezeko la watoto mitaani na madhara mengine mengi


                                        ---Image result for SHINYANGA

Wametaja sababu zinazopelekea wanafunzi kupata ujauzito kuwa ni kukosa hofu ya mungu,vishawishi,lakini pia wazazi kukumbatia mila kandamizi inachangia, Pamoja na sababu nyinginezo.

Mmoja wa wanafunzi hao Yohana Bartazar Kija ameomba mamlaka zinazohusika na maamuzi kuhakikisha zinazimamia sheria ikiwa ni Pamoja na kudhibiti mianya ya rushwa  ili kuwabana watuhumiwa wanaohusika na matukio hayo
.
Kwa upande wake makamu mkuu wa shule ya sekondari Buluba mwalimu MAKOYE NZALA amesema Pamoja na vyanzo vingine lakini utandawazi ni moja ya sababu zinazowasababishia wanafunzi kupata ujauzito.

                                    …..
Mwalimu NZALA  ameomba elimu ya Jinsia iendelee kutolewa hasa mashuleni kuhusu madhara ya kujihusisha na mapenzi katika umri mdogo

No comments