Header Ads

Wanafunzi wa kidato cha nne Nchini kote wanatarajiwa kuanza mitihani yao ya mwisho,siku ya Jummane Novemba mosi mwaka huu

Wanafunzi wa kidato cha nne Nchini kote wanatarajiwa kuanza mitihani yao ya mwisho,siku ya  Jummane Novemba mosi mwaka huu ambapo wametakiwa  kutumia muda wao kujiandaa,badala ya kuhangaika kufanya  udanganyifu wa kutafuta mitihani.
Hayo yamebainishwa na makamu mkuu wa shule ya Sekondari Buluba iliyopo katika manispaa ya Shinyanga Mwalimu MAKOYE NZALA wakati akizungumza na KALI ZOTE BLOG

Image result for picha za shule ya sekondari tosamaganga
                                     COPY KWENYE MTANDAO

Amesema  wanafunzi wanapaswa kutumia muda wao kujiandaa na kuomba ushauri wa kitaaluma kutoka kwa walimu,badala ya kuhangaika kutafuta mitihani  hali ambayo itawapotezea muda, kwani mitihani watakayopatiwa mitaani  ni bandia
                        --
Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Buluba iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga wamesema wana uhakika wa kufanya vizuri mitihani yao kwani wamejiandaa vyema.
                                         ----
Makamu mkuu wa shule ya Sekondari Buluba ametoa angalizo kwa wanafunzi kutojihusisha na udanganyifu katika kipindi chote  ambacho mitihani inaendelea kwani vyombo vya usalama havitosita kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wahusika.
                                                                    





No comments