Header Ads

Watanzania wapatao milioni 1.4 wanaishi na vvu

Watanzania  wapatao milioni 1.4 wanaishi na vvu


 
Hayo yameelezwa katika taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto ambapo imesema ilianza kutoa huduma za VVU na UKIMWI kwa makundi hayo maalum tangu mwaka 2010 baada ya kufanya tafiti na kugundua kuwa kiwango cha maambukizi ya VVU kiko juu kwenye makundi hayo.

Serikali imeyataja makundi yaliyopo hatarini zaidi kwa maambuki hayo ni pamoja na wasichana na wavulana, walio katika umri wa balehe, watoto yatima na watoto walio katika mazingira hatarishi, wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao, wanawake wanaofanya ngono kinyume na maumbile, watu wanaotumia dawa za kulevya kwa njia ya kujidunga sindano.

Takwimu zinaonyesha kuwa takribani watu 1,400,000 wanaishi na VVU nchini Tanzania ambapo, watu 839,574 wanapatiwa tiba ya dawa za kupunguza makali ya VVU zinazotolewa katika vituo ambapo takriban vituo 4,000 vilikuwa vinatoa huduma hiyo nchi nzima hadi kufikia mwezi Juni mwaka huu (2016

No comments